Thursday, July 10, 2014

WATAFITI SOMALIA, UHARAMIA HUENDA UKAPUNGUA!



Utafiti wa hivi karibuni unaashiria kwamba uharamia kutoka pwani ya Somalia huenda ukapungua kwa kiwango kikubwa kwa kuwapatia wazee wa koo za kisomali njia mbadala za kujikimu kimaisha. Kwa mujibu wa ripoti ya utafiti huo wa chuo kikuu cha Oxford na King's College mjini London, iliyochapishwa katika jarida moja la Uingereza, Jamii huwalinda maharamia wakati hawana njia nyengne za kujipatia kipato.
Kwa sasa Jamii ya kimataifa inategemea mikakati iliyo ghali mno, zikiwemo meli za kijeshi kuzuia uhaharamia wa majini na kuweka njia za safari za majini kuwa salama .
Lakini utafiti huu unakubaliana na yale ambayo yamekuwa yakipendekezwa na wadau mbalimbali Afrika mashriki, kwamba suluhu la kudumu ni kujenga miundo mbinu kama vile bandari na barabara zitakazo wawezesha wanavijiji wa koo mbalimbali wanufaike kwa fursa za kibiashara halali, zitakazowawezesha kupata tiza za kuendeleza maisha yao.

Related Posts:

  • KANYE ASHTAKIWA KWA ULAGHAIShabiki mmoja ameamua kumshtaki nyota wa muziki wa Rap Kanye West pamoja na huduma ya muziki ya Tidal kuhusu kutolewa kwa albamu mpya ya mwanamuziki huyo,The life of Pablo. Justin Baker-Rhett anadai alidanganywa kutia saini n… Read More
  • REFA MAREHEMU KUAMUA MECHIMwanamume aliyefariki ameteuliwa kusimamia mechi ya soka nchini Nigeria ambayo itachezwa Jumapili, mwandishi wa BBC anayefuatilia masuala ya soka Oluwashina Okeleji anasema. Wale Akinsanya aliteuliwa kuwa mwamuzi kwenye mechi… Read More
  • DONALD TRUMP AAHIDI KUJIBADILISHIA SIFAMgombea wa urais nchini Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican Donald Trump ameahidi kubadilisha sifa zake katika mkutano wa faragha na viongozi wa Republican. Mfanyibishara huyo ambaye yuko kifua mbele katika kuwania ur… Read More
  • MKATABA WA LUGUMI WAJADILIWA BUNGENIHATIMAYE taarifa ya utekelezaji wa mkataba tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises, iliyoshinda zabuni mwaka 2011 ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya Polisi vya wilaya nchi nzima kwa gharama ya Sh bi… Read More
  • MAJAMBAZI WAUA KWENYE TUKIO LA UPORAJI SUPPERMARKETWAKAZI wanne wa jijini Tanga wamekufa papo hapo na wengine wawili kujeruhiwa kwa risasi na majambazi . Majambazi hao waliokuwa na bunduki aina ya SMG , walivamia juzi duka kuu (supermarket) la mfanyabiashara Hamoud Ali lililo… Read More

0 comments:

Post a Comment