Thursday, July 10, 2014

JAJI MUTUNGI APEWA TAHADHARI NA CHADEMA MTWARA



Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi apewa tahadhali kali na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mtwara, kuacha  kukiingilia chama katika katiba yake kwa kutoa taarifa zenye lengo hasi kwa maendeleo na ukuaji wa demokrasia nchini
Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo mkoani mtwara, Kasim Bingwe alisema Jaji Mutungi kukiingilia chama hicho katika shughuli zake za halali ni kinyume na majukumu ya ofisi yake kwa mujibu wa sheria na matarajio ya wananchi katika kujenga demokrasia nchini.
“Msajili anatambua kuwa huu ni ubakaji wa demokrasia na pia anaendelea kutolea hoja mambo yasiyo na mashiko huku akinyamazia mambo yanayolalamikiwa kukwaza demokrasia nchini, licha ya msajili kudai amepokea malalamiko ya wanachama wa CHADEMA wakiwemo waliofukuzwa, iweje ayatoe leo kwenye vyombo vya habari huku akijua kuwa kifungu kinacholalamikiwa kilifutwa na katiba mpya ya 2006?” alihoji.
Mwenyekiti  huyo wa chama cha demokrasia na maendeleo mheshimiwa Bingwe aliongezea kwa kusema:
 “Hivi msajili ameshindwa kuona kuwa wanachama wa chama cha CCM wameanzisha na kuendeleza kampeni za uchaguzi wa 2015 kabla ya wakati huku akijua kuwa hilo ni kinyume cha Katiba na sheria ya uchaguzi?.....inaonekana msajili haoni vijembe vya makundi ndani ya CCM kugombea uongozi kwenye chama chao kabla hata ya muda jambo lililosababisha baadhi yao kuadhibiwa.
Anaongeza kuwa kitendo cha msajili kutamka kuwa mazuio kwa uongozi wa CHADEMA kujihusisha na mambo ya chama kumezua mtafaruku miongoni mwa wanachama na miongoni mwa wapenda chama, hivyo kuwaweka katika hali tete.
“Jambo hili limetusababishia usumbufu wa kujibu mambo yasiyo na tija kwa jamii huku tukiacha kutekeleza majukumu ya ndani ya chama na jamii katika ujenzi wa demokrasia na uchumi wa jamii,” alisema Bingwe.
Hivi karibuni msajili alinukuliwa akizungumza na vyombo vya habari akikaripia na kuwazuia viongozi wakuu wa Chadema kutogombea tena nyadhifa zao, kwani kwa kufanya hivyo ni kuvunja katiba ya chama hicho.

Related Posts:

  • WAPENZI JINSIA MOJA WATAHADHARISHWA UKSerikali ya Uingereza imewaonya wapenzi wa jinsia moja wanaosafiri kuelekea Marekani kutokana na sheria dhidi yao katika majimbo ya North Carolina and Mississippi. Marekani ni jamii kubwa ilio na maoni tofauti.Sheria mpya zil… Read More
  • MADAWA HARAMU, E.P.LSerikali ya Uingereza imeanzisha uchunguzi wa dharura kufuatia ufichuzi kuwa wachezaji nyota wa kandanda nchini Uingereza wamekuwa wakitumia madawa yaliyopigwa marufuku ya kuongeza nguvu mwilini. Gazeti la Sunday Times limech… Read More
  • MAKUBALIANO YA SYRIA MATATANIRais Barack Obama wa Marekani pamoja na mjumbe wa Umoja wa mataifa nchini Syria Staffan Di Mistura wamesema kuwa wanahofia kwamba makubaliano ya Syria huenda yakaanguka. Katika ghasia za hivi karibuni,watu 18 wamefariki kufua… Read More
  • SERIKALI YAPONGEZWA NA SHIRIKISHO LA WAFANYAKAZI ZANZIBARSHIRIKISHO la Vyama Huru vya Wafanyakazi Zanzibar (ZATUC) limeelezea kuridhishwa na juhudi zinazochukuliwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya kutekeleza mapendekezo yake, ikiwemo kuundwa kwa chombo cha majadiliano kitaif… Read More
  • BOMBA LA MAFUTA KUPATA UAMUZI MWISHONI MWA WIKIViongozi wa Kenya, Uganda na Tanzania mwishoni mwa wiki wanatarajiwa kutoa uamuzi wa mwisho kuhusu ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Uganda na Kenya hadi pwani. Mwaka jana, Kenya na Uganda zilikuwa zinashauri… Read More

0 comments:

Post a Comment