Monday, May 2, 2016

Mzazi wa watoto watatu aomba msaada; Pumu yamuandama



MKAZI wa Kijiji cha Mapinduzi Kata ya Kigwe Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma

Julietha Sokoine (24) ambaye amejifungua watoto wa watatu na ameiomba serikali,taasisi,mashirika  na watu binafsi kumpatia msaada wa kifedha utakaomsaidia kuwatunza watoto hao.

 Pia alisema msaada huo pia utamuwezesha kupata tiba ya ugonjwa wa pumu

ambao umemsababisha kuvimba mwili wote.

 Akizungumza mwishoni mwa wiki, Sokoine ameiomba jamii kumsaidia kutokana na

kukabiliwa na tatizo la ugonjwa wa pumu ambao pia umesababishia kuwa na

hali ngumu ya kimaisha ambayo inayomfanya kushindwa kuwatunza vizuri watoto

wake hao.

 Alisema watoto hao, Daniel Sokoine,David Sokoine na Davis Sokoine

walizaliwa kwa pamoja Machi 22, mwaka huu katika hospitali ya mkoa wa

Dodoma huku kati ya wawili wa wakiwa na uzito kilo mbili na nusu na wa

mwisho kilo mbili.

  “Hali yangu siyo mzuri kutokana na mimi mwenyewe kukabiliwa na tatizo la

ugonjwa wa pumu,ambao pia wakati mwingine ninalazimika kuwanywesha maziwa

ya ngombe watoto hao pindi ninapozidiwa na ugonjwa huo”alisema .

 Kwa upande wake baba wa watoto hao Sokoine Chipanta alisema pamoja na

juhudi nilizofanya za kilimo hata hivyo mazao yalinyauka na jua.

 Alisema kutokana na hali hiyo analazimika kutafuta vibarua ili kuweza

kupata fedha kwa ajili ya kununua chakula pamoja na matunzo ya watoto hao.

 Alisema kwa wale wote watakaoguswa na kuamua kumpa msaada wawasiliane naye

kwa namba ya simu 0652-744510.

Related Posts:

  • NAPE AZINDUA TAMASHA LA KIMATAIFA LA FILAMU MJINI ARUSHA  Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza wakati wa uzinduzi wa tamasha la Kimataifa la Filamu la Tanzanite mkoani Arusha .  Waziri Nape aliwaambia wadau na waigizaji wa Filamu wali… Read More
  • BURIANI PAPA WEMBA Nyota wa muziki wa Soukous ambaye ni raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo- Papa Wemba amefariki dunia Papa Wemba ambaye jina lake halisi ni Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba, alianguka na kufa jukwaani akiwatumbuiza ma… Read More
  • UGANDA: BOMBA LA MAFUTA KUPITIA TANZANIA Uganda imeamua kujenga bomba la mafuta yake kupitia Tanzania na wala sio Kenya. Awali taifa hilo la Afrika mashariki ambayo haijapakana na bahari ilikuwa imezungumzia nia ya kujenga bomba la mafuta yake kupitia Kenya lakini … Read More
  • TWITTER YAMTIA NDANI MWANDISHI Polisi nchini Uturuki wamekamata mwandishi wa habari aliyemkosoa rais wa nchi hiyo kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter. Ebru Umar raia wa Uholanzi alikamatwa na polisi baada ya kumkosoa rais Recep Tayyip Erdogan alikamatwa… Read More
  • UKIMYA WA UPINZANI BUNGENI MASHAKA KWA WASOMI UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu wakati wa mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, umechukuliwa kwa hadhari kuwa unaweza kusababisha kambi hiyo ionekane inalinda posho bu… Read More

0 comments:

Post a Comment