Monday, May 2, 2016

MWALIMU AKIMBIA NA MSHAHARA WA MWAKA

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Stephen Kebwe ameamuru kukamatwa kwa Mwalimu Hamisi Salumu Mkoleme kwa tuhuma za kulipwa mishahara ya mwaka mmoja na nusu bila kufanya kazi katika kituo chake alichopangiwa baada ya uhamisho kutoka mkoa wa Tanga kwenda mkoa wa Morogoro bila kuripoti katika kituo alichopangiwa.

Akizungumza na walimu waliofika katika ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Mvomero ili kuhakikiwa Mkuu huyo wa Mkoa wa Morogoro Dokta Kebwe Stephen Kebwe ameitaka kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Mvomero kusimamia kwa ukamilifu zoezi hilo ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wenyewe kutoa ushirikiano katika zoezi hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa amesema wameamua kuchukua hatua za kupitia upya orodha aliyokabidhiwa na Halmashauri ili kujiridhisha na kwamba iwapo itabainika mwalimu yeyote amefanya kosa kama hilo, hatua kali zitachukuliwa.

Related Posts:

  • MAJAMBAZI WAUA KWENYE TUKIO LA UPORAJI SUPPERMARKETWAKAZI wanne wa jijini Tanga wamekufa papo hapo na wengine wawili kujeruhiwa kwa risasi na majambazi . Majambazi hao waliokuwa na bunduki aina ya SMG , walivamia juzi duka kuu (supermarket) la mfanyabiashara Hamoud Ali lililo… Read More
  • KANYE ASHTAKIWA KWA ULAGHAIShabiki mmoja ameamua kumshtaki nyota wa muziki wa Rap Kanye West pamoja na huduma ya muziki ya Tidal kuhusu kutolewa kwa albamu mpya ya mwanamuziki huyo,The life of Pablo. Justin Baker-Rhett anadai alidanganywa kutia saini n… Read More
  • DONALD TRUMP AAHIDI KUJIBADILISHIA SIFAMgombea wa urais nchini Marekani kwa tiketi ya chama cha Republican Donald Trump ameahidi kubadilisha sifa zake katika mkutano wa faragha na viongozi wa Republican. Mfanyibishara huyo ambaye yuko kifua mbele katika kuwania ur… Read More
  • MKATABA WA LUGUMI WAJADILIWA BUNGENIHATIMAYE taarifa ya utekelezaji wa mkataba tata wa Kampuni ya Lugumi Enterprises, iliyoshinda zabuni mwaka 2011 ya kufunga mashine za kuchukua alama za vidole katika vituo vya Polisi vya wilaya nchi nzima kwa gharama ya Sh bi… Read More
  • REFA MAREHEMU KUAMUA MECHIMwanamume aliyefariki ameteuliwa kusimamia mechi ya soka nchini Nigeria ambayo itachezwa Jumapili, mwandishi wa BBC anayefuatilia masuala ya soka Oluwashina Okeleji anasema. Wale Akinsanya aliteuliwa kuwa mwamuzi kwenye mechi… Read More

0 comments:

Post a Comment