Thursday, July 10, 2014

WEMA SEPETU, KAJALA MASANJA BIFF KUSHNEY!!



Muigizaji wa filamu nchini, Wema Sepetu, amesema amefurahi kurudiana ‘ushosti’ na muigizaji mwenzake, Kajala Masanja, Wema alisema pamoja na Kajala kumkosea ila amefurahi kuwa naye karibu kwani alikuwa anakwazika na hasa alipokuwa anasikia habari zake kwa watu wa karibu na Kajala.
“Nashukuru Mungu hili bifu limeisha kiukweli, nimefurahi sana kwani nilikuwa nakwazika kila nikipata habari za Kajala kwa watu wake wa karibu, kiukweli nimefurahi,” alisema Wema.
Wema Sepetu na Kajala walikuwa na bifu lililokuwa linadhaniwa haliwezi kumalizika hadi kufikia hatua ya kuundwa kwa makundi yanayodaiwa ya kiuchochezi baina yao.

0 comments:

Post a Comment