• This is Slide 1 Title

    This is slide 1 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 2 Title

    This is slide 2 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 3 Title

    This is slide 3 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

Monday, May 2, 2016

GETRUDE CLEMENT AREJEA: BUNGE LAMKARIBISHA


Getrude Clement mwenye umri wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu anayesoma shule ya Sekondari Mnarani iliyopo jijini Mwanza, leo amepata nafasi ya kufika bungeni Dodoma baada ya kupewa mwaliko wa Serikali 

Hivi karibuni Getrude  alihutubia viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa uliohusu mabadiliko ya tabia nchiuliofanyika New York Marekani ambapo leo Bungeni  amewahimiza Watanzania kutunza mazingira na kufuata maelekezo yanayotolewa na Serikali na wataalamu wa mazingira ili kuyatunza mazingira wanamoishi.

Getrude amesema kuwa amefarijika kwa kuwawakilisha vijana wa Tanzania na dunia kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ambapo mataifa 175 yalikutana kusaini makubaliano ya Paris.

Katika kuwahimiza vijana kujenga tabia ya kutunza mazingira, Getrude amewaasa vijana hasa wanafunzi kusimamia suala la utunzaji wa mazingira wakiwa shuleni kwa kwa kujiunga na klabu mbalimbali ambapo yeye amejiunga na klabu ya “Mali Hai” iliyopo shuleni anaposoma.

Kwa upande wa Watanzania kwa ujumla kwenye utunzaji wa mazingira, Getrude amesema kuwa ni vema wajifunze kutoka mataifa mengine yanavyosimamia utunzaji wa mazingira hasa matumizi ya mifuko ya plastiki.

Mwanafunzi huyo amekaribishwa na kutambulishwa kwa wabunge leo mjini Dodoma kwa heshima ya kuliwakilisha vema taifa wakati wa utiaji saini makubaliano ya namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki moon alimkaribisha Getrude kwa viongozi hao na kusema “Ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni mwakilishi wa vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha sauti za vijana”.

MWALIMU AKIMBIA NA MSHAHARA WA MWAKA

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Stephen Kebwe ameamuru kukamatwa kwa Mwalimu Hamisi Salumu Mkoleme kwa tuhuma za kulipwa mishahara ya mwaka mmoja na nusu bila kufanya kazi katika kituo chake alichopangiwa baada ya uhamisho kutoka mkoa wa Tanga kwenda mkoa wa Morogoro bila kuripoti katika kituo alichopangiwa.

Akizungumza na walimu waliofika katika ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Mvomero ili kuhakikiwa Mkuu huyo wa Mkoa wa Morogoro Dokta Kebwe Stephen Kebwe ameitaka kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Mvomero kusimamia kwa ukamilifu zoezi hilo ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wenyewe kutoa ushirikiano katika zoezi hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa amesema wameamua kuchukua hatua za kupitia upya orodha aliyokabidhiwa na Halmashauri ili kujiridhisha na kwamba iwapo itabainika mwalimu yeyote amefanya kosa kama hilo, hatua kali zitachukuliwa.

Mzazi wa watoto watatu aomba msaada; Pumu yamuandama



MKAZI wa Kijiji cha Mapinduzi Kata ya Kigwe Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma

Julietha Sokoine (24) ambaye amejifungua watoto wa watatu na ameiomba serikali,taasisi,mashirika  na watu binafsi kumpatia msaada wa kifedha utakaomsaidia kuwatunza watoto hao.

 Pia alisema msaada huo pia utamuwezesha kupata tiba ya ugonjwa wa pumu

ambao umemsababisha kuvimba mwili wote.

 Akizungumza mwishoni mwa wiki, Sokoine ameiomba jamii kumsaidia kutokana na

kukabiliwa na tatizo la ugonjwa wa pumu ambao pia umesababishia kuwa na

hali ngumu ya kimaisha ambayo inayomfanya kushindwa kuwatunza vizuri watoto

wake hao.

 Alisema watoto hao, Daniel Sokoine,David Sokoine na Davis Sokoine

walizaliwa kwa pamoja Machi 22, mwaka huu katika hospitali ya mkoa wa

Dodoma huku kati ya wawili wa wakiwa na uzito kilo mbili na nusu na wa

mwisho kilo mbili.

  “Hali yangu siyo mzuri kutokana na mimi mwenyewe kukabiliwa na tatizo la

ugonjwa wa pumu,ambao pia wakati mwingine ninalazimika kuwanywesha maziwa

ya ngombe watoto hao pindi ninapozidiwa na ugonjwa huo”alisema .

 Kwa upande wake baba wa watoto hao Sokoine Chipanta alisema pamoja na

juhudi nilizofanya za kilimo hata hivyo mazao yalinyauka na jua.

 Alisema kutokana na hali hiyo analazimika kutafuta vibarua ili kuweza

kupata fedha kwa ajili ya kununua chakula pamoja na matunzo ya watoto hao.

 Alisema kwa wale wote watakaoguswa na kuamua kumpa msaada wawasiliane naye

kwa namba ya simu 0652-744510.

Punyeto yamfukuzisha kazi Waziri wa Wizara ya Mawasiliano Enock Ruberangabo



Rais Jamhuri wa Kidemokrasi ya Congo, Joseph Kabila amemtimua kazi Naibu Waziri wa Posta na Mawasiliano kutokana na kusambaa kwa video inayomuonesha akipiga punyeto ofisini

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa, RTNC, Kabila amedai waziri huyo, Enock Ruberangabo Sebineza ameliabisha taifa.
 

Tangu Alhamis iliyopita hadi Ijumaa, video hiyo imekuwa ikisambaa mtandaoni ikimuonesha waziri huyo akijichua ofisini kwake. Nyuma yake inaonekana bendera ya nchi hiyo na picha ya Rais Kabila.
 

Wananchi wengi wamekasirishwa na video hiyo na kumtaka ajiuzulu.

Saturday, April 30, 2016

WAPINZANI WABUNI MBADALA WA KURUSHA YANAYOJIRI BUNGENI

Wabunge wa CCM jana waliibuka kidedea walipowazidi wenzao wa upinzani kwa kura za sauti “Siyooooo” kuikataa hoja ya kutaka matangazo ya Bunge kurushwa moja kwa moja ‘live’ na televisheni. 

Hiyo ilitokea jana wakati Bunge lilipokaa kama kamati kupitisha bajeti ya Ofisi ya Rais (Tamisemi na Utumishi na Utawala Bora) na kuzua mvutano mkali uliosababisha bajeti hiyo ipitishwe kwa utaratibu wa wabunge kutohoji kitu chochote (guillotine).

Wakati hoja yao hiyo ikipingwa kila kona, tangu kuanza kwa Bunge la Bajeti, wabunge hao wa upinzani sasa wamebuni mbinu mpya ya kujirekodi wenyewe wakati wakichangia mijadala mbalimbali bungeni na kurusha sauti zao kwenye mitandao ya kijamii na kupeleka sauti hizo kwenye redio zilizopo katika maeneo ya majimbo yao.

Mbunge wa Malindi (CUF), Ally Salehe ndiye aliyeibua hoja hiyo akitaka kushika mshahara wa waziri kwa maelezo kuwa kuzuia Bunge kurushwa ‘live’ ni kinyume na utawala bora na haki ya kupata habari.

Hoja hiyo iliungwa mkono na  Mbunge wa Iringa Mjini (Chadema), Mchungaji Peter Msigwa, Masoud Abdalla Salim (Mtambale-CUF), Rose Kamili (Viti Maalumu -Chadema), Ester Matiko (Tarime Mjini – Chadema) na Mussa Mbarouk (Tanga Mjini - CUF).

Wabunge wa CCM waliopewa nafasi na Mwenyekiti wa Bunge, Andrew Chenge kuchangia hoja hiyo ni Peter Serukamba (Kigoma Kaskazini), Kangi Lugola (Mwibara), Hawa Ghasia (Mtwara Vijijini) pamoja na Waziri Ofisi ya Rais - Utumishi na Utawala Bora, Angela Kairuki.

Ilivyokuwa  Bungeni

 Baada ya Salehe kutaka ufafanuzi wa kina huku akisisitiza kuwa uamuzi huo unakiuka Katiba ya nchi na haki ya kupata habari, Kairuki alisema kwa mujibu wa Ibara ya 18 na 100 ya Katiba zinazozungumzia uhuru wa kupata habari, uamuzi huo ni sahihi na hakuna mwananchi aliyenyimwa taarifa.

Maelezo hayo yalipingwa na Salehe, safari hii akifafanua kuwa matangazo ya Bunge yanarekodiwa kwa saa saba na kurushwa na Televisheni ya Taifa (TBC) kwa saa moja tu, huku wabunge wa upinzani wakiondolewa na kuonyeshwa wa CCM pekee.

Alitaka vyombo vya habari vya elektroniki kuruhusiwa kurekodi shughuli za Bunge na kurusha maudhui wanayoyataka, badala ya kupewa video na studio ya Bunge ambayo huondoa michango na hoja za wapinzani.

Mchungaji Msigwa, Masoud Abdallah, Kamili, Matiko waliungana na Salehe na kusisitiza kuwa nchi nyingi barani Afrika zinarusha ‘live’ matangazo ya Bunge huku wakihoji sababu za TBC kurusha moja kwa moja harusi na kushindwa kuonyesha shughuli za Bunge.

Mbarouk alikwenda mbali akitaka Bunge kuanza shughuli zake usiku ili kuendana na utetezi wa Waziri wa Habari, Nape Nnauye kuwa usiku wananchi wengi wanakuwa majumbani mwao hivyo wanapata nafasi nzuri ya kufuatilia Bunge.

Matiko: Juzi Rais John Magufuli kazindua Daraja la Kigamboni, TBC ilikata matangazo ya Bunge ili kuonyesha uzinduzi huo. Yaani ya kwenu mnataka yaonyeshwe ila haya ya Bunge yasionekane. Mnakiuka demokrasia.

Ghasia: Demokrasia siyo Bunge kuonyeshwa ‘live’. Wakulima na wafugaji hawawezi kuona Bunge asubuhi ndiyo maana yanarushwa usiku. 

Serukamba: Mbona wabunge wa Chadema wanaonyeshwa katika matangazo ya TBC. Hoja kwamba maagizo ya Serikali hayatawafikia watendaji si kweli.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), George Masaju alisema wapinzani hawajiamini na hawaaminiki huku akiwataka wasome ibara ya 100 ya Katiba; “Bunge kuonyeshwa au kutoonyeshwa hakuongezi kitu jimboni. Wanaozungumza ni wabunge siyo televisheni.”

Akihitimisha hoja, Kairuki alipinga maelezo ya Salehe na kutoa mfano wa nchi ambazo matangazo ya Bunge hayarushwi moja kwa moja.

Kutokana na mvutano huo Chenge aliwahoji wabunge wanaoafiki hoja ya Salehe waseme “ndiyooo”, wapinzani pekee wakasema ndiyoo, aliposema wasioafiki waseme siyo, wabunge wa CCM kutokana na wingi waliitikia kwa sauti kubwa siyoooo, na Chenge akasema anadhani wasioafiki wameshinda. 

Wapinzani  Waamua Kujirekodi kwa simu

Kwa zaidi ya mara tano,wabunge wa upinzani wameshuhudiwa wakijirekodi ndani ya ukumbi wa Bunge kwa kutumia simu zao za mkononi, wanapotoka nje huulizana kama wameshatumia video na sauti hizo katika mitandao ya kijamii.

Juzi, Mbunge wa Ukonga (Chadema), Mwita Waitara baada ya kumaliza kuchangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais (Tamisemi na Utawala Bora) alirusha sauti yake katika mitandao ya kijamii na kusema hiyo ni moja ya njia ya kuwafanya wananchi wajue kinachoendelea bungeni.

465 KUSUBIRI KUNYONGWA

IDADI ya Watanzania wanaosubiri kunyongwa imekuwa ikiongezeka na hadi sasa imefikia 465 kutokana na hukumu ya kifo kutotekelezwa tangu mwaka 1994. 

Ripoti iliyotolewa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora katika mafunzo kwa waandishi wa habari mjini Morogoro juzi, imebainisha kuwa hakuna hukumu yoyote ya kifo iliyosainiwa na Rais ili kutekelezwa hadi Oktoba 2015 kulipofanyika Uchaguzi Mkuu ambao Rais Magufuli aliibuka mshindi.

Ripoti hiyo ya Mpango wa Kujitathmini Kuhusu Hali ya Utekelezaji wa Haki za Binadamu (UPR), unaotekelezwa kwa mara ya pili nchini, imeonesha kuwa kuna mahabusu 465 wanaosubiri adhabu ya kifo, kati yao wanaume ni 445 na wanawake ni 20.

Wanaharakati 

Akiwasilisha ripoti hiyo, Ofisa Uchunguzi Mkuu wa Tume hiyo, Philemon Mponezya, alisema Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, inaitaka Serikali kufuta adhabu hiyo kwa kuwa haitekelezeki lakini baadhi ya asasi hasa zinazohusika na haki za walemavu wa ngozi, zinapinga kufutwa kwa adhabu hiyo.

Baadhi ya asasi zinazopinga kufutwa kwa hukumu ya kifo ni taasisi ya Under The Same Sun (UTSS), ambayo inasema katika utafiti waliofanya, wahusika wanataka hukumu hiyo hasa inayohusu watu walioua albino, itekelezwe mpaka hapo mauaji hayo yatakapokoma.

Hata hivyo, Mponezya alisema watetezi wengi wa haki za binadamu wanataka adhabu hiyo ifutwe kwa kuwa ni kinyume cha haki za binadamu na kwa Tanzania, imekuwa mbaya zaidi kwa kuwa baadhi ya wahukumiwa wamesubiri zaidi miaka 20 bila hukumu dhidi yao kutekelezwa, jambo linalowaathiri kisaikolojia.

“Tume inasisitiza Serikali iangalie upya hukumu hii na kuiondoa kwa sababu ya utekelezaji wake. Tangu mwaka 1994 hadi leo watu 465 wanasubiri adhabu hiyo, hakuna aliyenyongwa. Kila mlango unapogongwa unahisi ni wewe kumbe la, tunadhani iondolewe maana haitekelezwi,” alisema Mponezya.

Wananchi wagawanyika 

Tume hiyo ilikiri kwamba, Tanzania imeshindwa kutekeleza adhabu hiyo kwa miaka mingi kutokana na Serikali kueleza kuwa jamii imegawanyika kuhusu hukumu hiyo. 

Wapo wanaotaka ifutwe lakini wengi wanataka iendelee kutekelezwa kutokana na ongezeko la mauaji ya vikongwe kwa imani za kishirikina na albino.

Wakili wa Serikali Mkuu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Mark Mulumbo, alipotakiwa kufafanua kuhusu mtazamo wa kisheria na kiserikali kuhusu utekelezaji wa adhabu hiyo katika mafunzo hayo, alikiri kwamba tafiti zilizofanywa nchini zimeonesha kuwa, kuna mgawanyiko kwa wananchi kuhusu adhabu hiyo.

“Tume kadhaa zilizoundwa kupata maoni ya wananchi, zilitoa matokeo kuwa wananchi wengi bado hawataki adhabu iondolewe, wanataka iendelee kuwapo, sasa Serikali inafanya kazi kwa matakwa ya wananchi, si vinginevyo,” alisema Mulumbo.

Akifafanua zaidi, alisema hata katika mchakato wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, hali hiyo ilijitokeza kwamba Watanzania wengi hawaoni kama muda ni mwafaka kufuta adhabu hiyo. 

Marais 

Kuhusu marais kushindwa kusaini hukumu hiyo, Mulumbo alisema upo mtazamo wa aina mbili kuhusu jambo hilo; wa kiimani na kisheria.

Alisema pamoja na kwamba nchi haina dini, marais wote waliowahi kuchaguliwa mpaka wa Awamu ya Tano, wana imani za kidini. 

“Siwasemei kwamba imani zao ni sababu, lakini huenda ni sababu.Ila kisheria rais hahukumiwi akisaini hukumu hiyo, sasa hilo mimi siwezi kulisemea ila sheria zinaweza kuangaliwa zaidi, ili zimpe rais nafasi ya kumpa mhusika kifungo cha maisha. 

“Lakini hapo napo kuna mtazamo mwingine, maana kuna hoja kwamba kwa nini aliyeua na kupatikana na hatia afungwe maisha. Je, iko wapi haki ya aliyeuawa?” Alifafanua Mulumbo kwa mtazamo wake.

Wanaoipenda 

Mwanasheria wa UTSS aliyewasilisha mada katika mafunzo hayo, Perpetua Senkoro, ambaye pia ana ulemavu wa ngozi, alisema  kwamba, utafiti uliofanywa na taasisi hiyo kwa walemavu wa ngozi (albino) kuhusu hukumu hiyo, umeonesha jamii inataka iendelee kuwapo, na itekelezwe.

Senkoro alisema wana imani sawa na wanaharakati wenzao wa haki za binadamu kuwa dhana ya hukumu ni kumfanya mkosaji abadilike na hukumu ya kifo haitoi nafasi ya kubadilika, lakini kwao kutokana na namna wanavyouliwa kwa imani za kishirikina, hilo si suala la tabia bali ni imani na hivyo muuaji hawezi kubadilika, wanaona heri iendelee kuwapo na itekelezwe.

“Wengi wa jamii yetu wanataka hukumu iendelee kuwapo mpaka hapo mauaji kwa albino yatakapokoma na itekelezwe. Wauaji wa albino wanaua kwa imani si tabia, wanatumwa na watu wenye fedha, kiungo kinauzwa Dola za Marekani 2,000, tena tunaona wanaokamatwa ni vidagaa, bado mapapa hatuyaoni, tunaomba Serikali (ya Magufuli) iwatafute vigogo na tuone hukumu hii ikitekelezwa ili kumaliza imani hizi zinazowanyima haki baadhi yetu ya kuishi,” alisema Senkoro.

Pamoja na Tanzania kuridhia mapendekezo kadha wa kadha ya haki za binadamu, bado Mei 9 hadi 12 mwaka huu, katika mkutano wa Geneva, Uswisi itaulizwa utekelezaji wa mapendekezo mengine na msimamo wa nchi kuhusu kufuta adhabu ya kifo.

Mkutano huo utahudhuriwa na asasi mbalimbali za utetezi wa haki za binadamu nchini, viongozi wa serikali pamoja na tume za haki za binadamu, ambapo nchi zaidi ya 190 zinatarajiwa kushiriki.

Ripoti mpya ya shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International, imeonesha kuwa idadi ya watu waliouawa mwaka 2015 katika utekelezaji wa hukumu ya kifo ni kubwa zaidi tangu mwaka 1990.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, watu 1,634 waliuawa mwaka jana sawa na asimilia 50 ya waliouawa mwaka 2014. Aidha takwimu hizo hazihusu utekelezaji wa hukumu hiyo nchini China, ambako takwimu za adhabu hiyo huwa siri ingawa zinatajwa kuwa kubwa. 

Nchi zinazotajwa kutekeleza zaidi hukumu hiyo mwaka jana ni Iran, Pakistan na Saudi Arabia ambako asilimia 90 adhabu hiyo ilitekelezwa.

Dr.MPANGO: Serikali ya JK haikukomba fedha Hazina

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dk Philip Mpango, amesema Serikali ya Awamu ya Nne iliyokuwa chini ya Rais Jakaya Kikwete haikukomba fedha katika Hazina kama ambavyo baadhi ya wabunge wamedai, hata Shirika la Kimataifa la Fedha (IMF), lilifanya tathmini na kutoa taarifa safi.

Dk Mpango alieleza hayo bungeni jana mjini hapa, wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na wabunge wakati wakichangia mjadala wa wizara mbili zilizo chini ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na Utawala Bora, Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

Katika mjadala huo, baadhi ya wabunge walisema Serikali ya Awamu ya Nne, ilikomba fedha zote Hazina na kusababisha Serikali ya Awamu ya Tano chini ya uongozi wa Rais John Magufuli, kukuta Hazina haina fedha.

Akijibu hoja hiyo, alisema hakuna ushahidi ulioitia hatiani Serikali ya Awamu wa Nne kuhusu kukomba fedha Hazina na kwamba IMF na wadau wengine wa kimataifa, walifanya tathmini huru ya bajeti na mwenendo wa uchumi nchini na taarifa yao ya mwisho waliitoa Desemba mwaka 2015.

Katika ripoti hiyo hakuna mahali ilipoonesha nchi ilikuwa na hali mbaya ya fedha na kwamba kwa kudhihirisha hilo, vigezo vya kimataifa vilionesha bayana kuwa Deni la Taifa ni himilivu na nchi bado inakopesheka na imeendelea kulipa mishahara watumishi wake pamoja na madeni mengine bila kutetereka.

Alisema Serikali iliendelea kulipa madeni mengi na hakuna kilicholegalega, huku ikiendelea pia kugharimia shughuli za mihimili yote, ikiwemo Bunge, usalama wa nchi na kuendelea kulipa madai ya makandarasi na watoa huduma wengine.

Alisema Serikali ya Awamu ya Tano imerithi mambo mengi mazuri yaliyofanywa na serikali za awamu zilizopita, ikiwemo uchumi imara, umeme uliosambazwa maeneo mengi vijijini na miundombinu.

8,236 HEWA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Angela Kairuki

SIKU chache baada ya Rais John Magufuli kutaja idadi ya watumishi hewa kuwa ni 7,200, msako unaoendelea katika utumishi wa umma, umetoa takwimu mpya ambapo sasa watumishi hao wamefikia 8,236.

Katika hatua nyingine, wakurugenzi wa halmashauri za wilaya ambao wamefunguliwa kesi mahakamani kutokana na ubadhirifu, ambao wamekuwa wanatumia magari na mafuta ya umma na kujilipa posho wanapokwenda kwenye kesi zao, wataanza kuchukuliwa hatua kali.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angela Kairuki, amesema hayo bungeni jana wakati akihitimisha hotuba yake ya bajeti kwa mwaka ujao wa fedha.

Akizungumzia wafanyakazi hewa, Waziri Kairuki alisema kati ya Machi Mosi na Aprili 24, mwaka huu, Serikali imebaini kuwepo kwa watumishi hewa 8,236, idadi inayoonesha kuwepo kwa ongezeko kubwa baada ya hivi karibuni Rais kuripoti kuwepo wafanyakazi hewa 7,200.

Alisema katika idadi hiyo, wafanyakazi hewa 1,614 wameripotiwa kutoka Serikali Kuu huku wengine 6,622 wakiripotiwa kutoka Serikali za Mitaa, na kufanya ongezeko lao kufikia 2,737.

Kwa mujibu wa Waziri Kairuki, kuwepo kwa wafanyakazi hao hewa katika utumishi wa umma kumeisababishia Serikali hasara ya Sh bilioni 15.4, ambazo zingeweza kutumika katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Alisema katika kushughulikia hilo, Serikali imelazimika kuwasimamisha kazi maofisa utumishi 56 ambao walibainika kuhusika kufanikisha malipo ya mishahara kwa watumishi hao hewa na hatua mbalimbali za kisheria zinaendelea kuchukuliwa dhidi yao.

‘’Hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa dhidi yao na endapo watabainika kuwa na makosa kisheria, watalazimika kurejesha fedha za Serikali zilizopotea kutokana na malipo hayo hewa ya mishahara,” alisema Kairuki.

Kuhusu wakurugenzi wa halmashauri wenye kesi za ubadhirifu mahakamani, Waziri Kairuki alisema Serikali inafanya uchunguzi kuhusu wakurugenzi hao ambao kutokana na kuwa na kesi mahakamani, wanatumia fedha na rasilimali za Serikali kwenda kuhudhuria kesi zao.

“Zipo taarifa hizo kwamba wakurugenzi hawa wanakwenda katika kesi hizo wakiwa wamejilipa posho za kujikimu za Serikali wao na madereva wao lakini pia wakitumia magari na mafuta ya Serikali. Ikibainika kuwa wapo wakurugenzi kama hawa hatua kali zitachukuliwa kwao mara moja,” alisema Waziri Kairuki.

Thursday, April 28, 2016

WATANO WAUWAWA MOROGORO KWA MAFURIKO


WATU watano wamefariki dunia na wengine 13,933 kutoka kaya 3,095 wameathiriwa baada ya kutokea kwa mafuriko makubwa ya mvua zilizonyesha maeneo mbalimbali ya wilaya za Kilosa, Kilombero, Morogoro na Wilaya mpya ya Malinyi mkoani Morogoro.

89 HEWA WABAINIKA: WALIPWA ZAIDI YA BILIONI 1


Aidha, Hapi amebaini uwepo wa watumishi vivuli 81 katika kada ya ualimu na hivyo kutoa siku saba kwa maofisa utumishi wa wilaya hiyo, kuhakiki watumishi vivuli ili kubaini idadi yao na hasara waliyosababisha.
Hapi aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam, na kueleza kuwa awali wakati akiingia katika ofisi yake wiki iliyopita alikuta kuna watumishi hewa 34 waliokuwa wamesababisha hasara ya Sh milioni 512.

NAIBU SPIKA: BWEGE BUNGENI


Naibu Spika Tulia Ackson, ambaye katika vikao vya Bunge anatakiwa kusimamia mijadala kwenye chombo hicho cha kutunga sheria, jana alizua kizaazaa baada ya kumuelezea mbunge wa Kilwa Kusini (CUF), Selemani Said Bungara kuwa ni bwege, akimtaka aache kuonyesha hali hiyo.

Wednesday, April 27, 2016

Vichwa vya Habari Magazeti ya leo April 28 Alhamisi

MALI ZA PRINCE ZAHITAJI USIMAMIZI


Nyota wa muziki wa Pop Prince hakuwacha wasia ,dadaake amefichua katika stakhabadhi za mahakama.
Nakala zilizowasilishwa katika mahakama ya jimbo la Minnesota zinaonyesha,Tyka Nelson ametoa ombi la mtu atakayesimamia mali ya nyota huyo.
Prince mwenye umri wa miaka 57 alipatikana amefariki katika lifti katika studio yake ndani ya makaazi ya Minneapolis,huko Minnesota Alhamisi iliopita.
Ukubwa wa mali yake haujulikani lakini unadaiwa kuwa dola milioni 27.

UDA: UCHUNGUZI UNAENDELEA


Wakati Serikali ikiendelea kuchunguza mikataba kati ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart) kuhusu Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ametia pilipili kidonda kwa kuibua udanganyifu unaolizunguka shirika hilo

POLISI ABAKA MWANAFUNZI


Mwanafunzi wa kidato cha tatu, juzi alimkaanga askari polisi anayedaiwa kumbaka kwa kuieleza Mahakama jinsi alivyotendewa kitendo hicho katika kibanda cha ulinzi cha benki.

Tuesday, April 26, 2016

TASAF: MAJINA HEWA MRADI WA KUOKOA KAYA MASIKINI


Wananchi wamemkataa mwenyekiti wa kitongoji cha Mwanogi kijiji cha Bulima, Kata ya Nyashimo wilayani Busega katika Mkoa wa Simiyu, wakimtuhumu kuweka majina hewa katika mradi wa kuokoa kaya masikini unaosimamiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).

3,551 WASAMEHEWA


Rais John Magufuli ametoa msamaha kwa wafungwa 3,551, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 52 ya Muungano wa Tanzania.

Monday, April 25, 2016

RUSHWA:OFISA WA TRA KIZIMBANI


Ofisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Amani Mkwizu na mfanyakazi wa kampuni ya udalali ya Yono Auction Mart, Edward Magobela wamepandishwa kortini jana wakikabiliwa na mashtaka matatu ya rushwa. 

ZITTO KABWE: MAKUNDI YA KIFISADI YAKABILIWE


Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe amemtaka Rais John Magufuli kukabiliana na vikundi vya mafisadi vinavyoiba mabilioni ya fedha za umma kupitia mikataba mibovu waliyoingia badala ya kuishia kutumbua majipu. 

Deni la Taifa Lafikia Trilion 33. 5



Deni la Taifa limeongezeka kwa Sh7.05 trilioni, kutoka Sh26.49 trilioni Juni 30, 2014, hadi Sh33.54 trilioni sawa na ongezeko la asilimia 27.

PICHA ZA UCHI ZAMFUNGA SIWEMA WA NEY WA MITEGO



Wiki iliyopita zilianza kusikika taarifa mbalimbali kuhusu kuhukumiwa kwa mpenzi wa zamani na mama mtoto wa msanii Nay wa Mitego aliyehukumiwa kwenda jela miaka miwili  jijini  Mwanza.

Afisa Uchaguzi Halmashauri Ya Serengeti Ahukumiwa Miaka Saba Jela.


AFISA uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara Bw.  Julius Bujabhi Makwasa amehukumiwa kifungo cha Miaka 7 jela baada ya kupatikana na hatia ya Makosa 34 yakiwepo ya Rushwa.

UBAKAJI WA KITHIRI INCHINI


Matukio ya ubakaji hasa kwa watoto wadogo yamekuwa yakiongezeka kwa kiwango kikubwa, ongezeko hili limebainika kutokana na ufuatiliaji tulioufanya kupitia matukio yaliyoripotiwa katika vituo vya Polisi

China Yakubali Kujenga Reli Ya Kati Kiwango Cha “Standard Gauge” Kilomita 2561


 CHINA imekubali kushirikiana na Tanzania katika utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa reli ya kati yenye urefu wa kilometa 2,561 kwa kiwango cha kisasa yaani "Standard Gauge"

Barabara ya Mwenge hadi Morocco Iliyojengwa Kwa Fedha za Sherehe za Uhuru Yakamilika kwa asilimia 95


Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Prof.Makame Mbarawa  amekagua  mradi wa upanuzi wa barabara ya Mwenge  hadi Morocco yenye kilomita 4.3 ambapo ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 95.

MAPENZI YAKATIZA UHAI WA MWANACHUO


Mwanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo Kikuu cha Elimu (Duce), jijini Dar es Salaam, Bertha Mwarabu (23), ameuawa na mwanafunzi mwenzake kwa kuchomwa kisu kwenye titi na tumboni kwa kinachodaiwa ni kutokana na wivu wa mapenzi.

SERA YA ELIMU BURE YATOLEWA UFAFANUZI


Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako, amewataka walimu na maafisa elimu kusimamia vyema majukumu yao na kuhakikisha utoaji elimu bora kwa wanafunzi ili kupata wataalamu watakaolisaidia taifa.

Breaking News :Rais Magufuli Ateua Makatibu Tawala wa Mikoa 26


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Aprili, 2016 amefanya uteuzi wa Makatibu Tawala wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara.

Sunday, April 24, 2016

TAKUKURU Kuchunguza Mabilioni ya Kikwete


ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imeanza kuchunguza fedha za uwezeshaji maarufu kama ‘Mabilioni ya JK’ ambazo hazikurejeshwa na wakopaji nchi nzima. 

Msemaji wa Takukuru, Tunu Mleli alisema jana kuwa taasisi hiyo imechukua jukumu hilo kwa sababu moja ya majukumu yake ni kuchunguza masuala ya rushwa na kutoa rai kwa mtu mwenye ushahidi au taarifa kuhusu suala hilo kuzitoa kwa taasisi hiyo.

“Takukuru ipo wazi kuzipokea taarifa hizo ili zitusaidie kwenye uchunguzi,” alisema Tunu.

Kati ya Sh50 bilioni zilizotolewa na Serikali ya Awamu ya Nne chini ya Rais mstaafu, Jakaya Kikwete, ni Sh43 bilioni tu zilizorejeshwa, huku Sh7 bilioni zikidaiwa kutafunwa. 

Fedha hizo zilitolewa na Kikwete kwa ajili ya kuwawezesha kimitaji, wajasiriamali nchi nzima, mikopo ambayo ilipitia benki za CRDB, NMB, Community Bank na Benki ya Posta Tanzania. 

Fedha hizo kutoka Mfuko wa Rais, zilikuwa zikikopeshwa kwa riba ya asilimia 10, ambapo asilimia mbili ilikuwa inaingia serikalini na nane ilikuwa inabaki kwenye benki hizo. 

Hata hivyo, baadhi ya vyama vya Akiba vya Kuweka na Kukopa (Saccos), vilivyopewa fedha hizo, vilitoa mikopo hiyo kiholela, huku baadhi ya viongozi wakidaiwa kutengeneza majina feki na kukopeshana fedha hizo. 

Imedaiwa kuwa Saccos nyingi ambazo zilifuja fedha hizo katika mikoa mbalimbali, viongozi wake wengi walikuwa pia ni viongozi wa kisiasa na wengine wakiwa na nyadhifa serikalini. 

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, baadhi ya waliokopeshwa fedha hizo na Saccos mbalimbali, hawakuwa wanachama, bali walichomekwa baada ya kuonekana kuna fursa ya ‘kupiga dili’.

Chanzo kutoka Takukuru, kimedokeza  kuwa makamanda wa taasisi hiyo katika mikoa mbalimbali, wamepewa maelekezo ya kuchunguza mahali yalipo mabilioni hayo na nani waliyafuja.

 “Ni kweli tumepewa maelekezo ya kuchunguza fedha hizo. Unajua hizi ni fedha za umma haziwezi kutafunwa tu hivihivi na Serikali ikakaa kimya,” alidokeza mmoja wa maofisa wa Takukuru. 

Machi mwaka jana, aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji), Christopher Chiza aliagiza kufanyika kwa ukaguzi wa kina wa fedha hizo.

Alitoa agizo hilo wakati wa ziara yake katika Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi (Neec), ambako aliagiza watakaobanika kuhusika na ubadhirifu wa fedha hizo wachukuliwe hatua za kisheria.

“Lazima tuangalie mabilioni ya JK yalipotelea wapi, yalivyofujwa na wahusika wapo wapi ili sheria ichukue mkondo wake. Nimeambiwa kuna zilizobaki tujue ziko wapi,”alikaririwa Chiza akisema. 

Lakini Desemba 24, 2013, mtangulizi wa Chiza, Mary Nagu alikaririwa akisema Sh43 bilioni kati ya Sh50 bilioni za mabilioni ya JK zilizokopeshwa kwa wajasiriamali 74,701 zilikuwa zimerejeshwa. 

Nagu alitoa takwimu hizo alipokuwa akizungumzia mafanikio ya Serikali ya Rais Kikwete katika, utaratibu uliofanywa pia na wizara nyingine. 

Suala la mabilioni hayo ya JK limekuwa likiibuka mara kwa mara bungeni na katika mitandao mbalimbali ya kijamii huku wananchi wakitaka zirejeshwe.

Mkataba wa Lugumi

Hii hapa ni taarifa ya Utekelezaji Ya Kamati Ndogo ya PAC Kuhusu Mkataba wa Lugumi


NAPE KUDILI NA MAJIPU KWENYE SANAA


Waziri wa Habari,Utamaduni,sanaa na michezo nchini,Nape Nnauye ametaja mambo manne ambayo ni vikwazo ndani ya sekta ya sanaa ya filamu nchini na kuyaita kwamba ni majipu huku akisisistiza kwamba serikali itakwenda kutunga sera ya sekta hiyo katika mwaka wa fedha 2016/17.

Nape,aliyataja mambo hayo na kuyafananisha na majipu kuwa ni uporaji wa kazi za wasanii nchini,ujenzi duni wa miundombinu ya kazi za wasanii nchini,usimamizi mbovu wa bodi ya filamu nchini sanjari na tatizo la mfumo mbovu wa usambazaji wa kazi za wasanii nchini.

Akizindua tamasha la filamu la Tanzanite International Film

Festival(TIFF) jijini Arusha juzi ambao ulihudhuriwa na wasanii maarufu wa filamu nchini waziri huyo alisema kwamba jipu la kwanza ambalo atakwenda kulitumbua ni uporaji wa kazi za wasanii nchini.

 

“Jipu la kwanza tutalitumbua kwenye bajeti yetu ya mwaka 2016/17 ni uporaji wa kazi za wasanii nchini wengi wananyonywa jasho lao”alisema

Nape

Hatahivyo,alisema kwamba jipu la pili ni ujenzi duni wa miundombinu ya kazi za wasanii za filamu nchini na kudai kwamba chini ya uongozi wake atahakikisha anaimarisha miundombinu bora kwa lengo la kuwasaidia wasanii hao pamoja na kulinda haki zao.

Alisema ya kwamba mfumo wa kazi za usambazaji wa kazi za wasanii nchini pamoja na hakimiliki ni wa kinyonyaji huku akitolea mfano wa kazi za msanii maarufu wa sanaa hiyo nchini marehemu Stephen Kanumba na kusema kwamba familia yake hainufaiki na matunda ya kazi zake hadi sasa kutokana na mfumo mbovu wa usimamizi wa kazi za wasanii nchini.

Alitaja takwimu kwamba mwaka 2011/12 jumla ya filamu 218

zilitengenezwa nchini na mwaka 2014/15 kazi hizo ziliongezeka hadi kufikia 14,00 huku akidai hilo linadhihirisha kwamba sekta hiyo inakua kwa kasi nchini na kuongeza ajira 
 

Hatahivyo,Rais wa shirikisho la wasanii wa filamu nchini(TAFF),Simon Mwakifamba aliwataka wasanii wa filamu nchini kujiandaa kisaikolojia kukabiliana na soko la ushindani wa filamu duniani kwa kuwa wabunifu.

“Serikali tunaiomba iandae sera itakayoandaa mazingira mazuri kwa wasanii nchini kuhusu usalama wa kazi zao”alisema Mwakifamba

Naye, muaandaji wa tamasha hilo,Said Sassi alisema kwamba tatizo la uharamia wa kazi za wasanii nchini limetanda na kuwaomba wafanyabiashara na makampuni kujitokeza kudhamini vipindi mbalimbali vya luninga kwa lengo la kuinua sekta hiyo.

Mkurugenzi wa kampuni ya uchimbaji wa madini ya vito ya Tanzanite One Mining Ltd ambao ni miongoni mwa wafadhili wa tamasha hilo,Feisal Shabhai alisema lengo la kampuni yao kujitosa kufadhili tamasha hilo ni kutoa mchango wao katika kusaidia jamii kupitia faida wanayoipata ili kuinua sekta ya ajira nchini.

KIZIMBANI KWA KUHIFADHI WAHAMIAJI HARAMU


Waziri wa Mambo ya Ndani, Charles Kitwanga.

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo, Simon Kagoli amefikishwa mahakamani kwa kosa la kuhifadhi wahamiaji haramu nyumbani kwake na kuwatumikisha mashambani.

Kagoli ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Kageji, anakabiliwa na mashitaka matatu ikiwemo kuishi na watu ambao sio raia, kuwasaidia raia wa kigeni kutenda kosa na kuajiri na kuwatumikisha wageni shambani mwake. Kesi hiyo namba 114/2016 iko mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Wilaya ya Kibondo, Robert Male.

Mwendesha Mashitaka wa Uhamiaji, Richard Mwangole alidai mshtakiwa alitenda kosa hilo kwa makusudi huku akijua kuwa kuhifadhi wahamiaji haramu ni kosa kubwa. Anatuhumiwa kuwafanyisha kazi wahamiaji hao na kuwalipa ujira wa Sh 110,000 kila mmoja. Male alikana makosa na yuko nje kwa dhamana.

Alidhaminiwa na wadhamini wawili, kila mtu kwa dhamana ya Sh milioni moja.

Serikali ya China kudhibiti dini

Chama cha kikoministi cha China kimepewa mamlaka ya kudhibiti dini nchini humo.

Kiongozi wa Uchina, Xi Jinping, amesema makundi ya kidini lazima yakubali kudhibitiwa na chama cha kikoministi.

Akizungumza katika mkutano wa siku mbili mjini Beijing,rais Xi alisema itikadi za dini lazima zifuate sheria na utamaduni wa Uchina.

Alisema dini haina mchango katika siasa za nchi.

Rais Xi piya alionya watu wa nje wanaingilia kati ya mambo ya taifa kwa kupitia njia za kidini.

Watu wa Uchina wanahimizwa kuhudhuria maeneo ya ibada yaliyokubaliwa na taifa na wanaweza kutiwa adabu kali wakifanya ibada kinyume cha sheria.

Serikali ya China kudhibiti dini

Chama cha kikoministi cha China kimepewa mamlaka ya kudhibiti dini nchini humo.

Kiongozi wa Uchina, Xi Jinping, amesema makundi ya kidini lazima yakubali kudhibitiwa na chama cha kikoministi.

Akizungumza katika mkutano wa siku mbili mjini Beijing,rais Xi alisema itikadi za dini lazima zifuate sheria na utamaduni wa Uchina.

Alisema dini haina mchango katika siasa za nchi.

Rais Xi piya alionya watu wa nje wanaingilia kati ya mambo ya taifa kwa kupitia njia za kidini.

Watu wa Uchina wanahimizwa kuhudhuria maeneo ya ibada yaliyokubaliwa na taifa na wanaweza kutiwa adabu kali wakifanya ibada kinyume cha sheria.

Wakenya kinara katika London Marathon

Mwanariadha mkenya Eliud Kipchoge nusura avunje rekodi ya duniaya mbio za Marathon alipoandikisha muda wa kasi zaidi katika mbio za London Marathon.

Kipchoge wa Kenya,alihifadhi taji aliloshindwa mwaka uliopita alipoandikisha muda wa kasi zaidi wa saa mbili dakika tatu na sekunde 5 sekunde 8 tu nje ya rekodi ya dunia ya mbio hizo.

Rekodi hiyo ya dunia iliwekwa na mkenya mwenza Dennis Kimetto katika mashindano ya Berlin Marathon mwezi Septemba mwaka wa 2014.

Kipchoge ambaye alikuwa ameandamana na mkenya mwenza Stanley Biwott hadi iliposalia takriban kilomita tatu kufikia kwenye utepe , alipotifua kivumbi na kubaini udedea wake katika mbio hizo za masafa marefu.

Biwott alijifurukuta na kumaliza katika nafasi ya pili huku mpinzani wake katika mbio za mita 5000 Kenenisa Bekele kutoka Ethiopia akifunga orodha ya tatu bora.

Kufuatia ushindi huo Kipchoge ndiye mwanariadha wa kwanza tangu Martin Lel vilevile wa Kenya aliposhinda taji lake la pili mwaka wa 2008.

Katika kitengo cha wanawake cha mbio hizo ,Mkenya mwengine, Jemima Sumgong, aliyeanguka katika sehemu ya mwanzo mwanzo wa mashindano ya leo alijitahidi na kuibuka mshindi wa mbio za wanawake.

Sumgong, 31, aligonga kichwa chake chini baada ya kutegwa na mwanariadha mpinzani kutoka Ethiopia Aselefech Mergia.

Hata hivyo alijifurukuta kutoika nyuma na kuandikisha muda wa saa mbili dakika 22 na sekunde 58 alipokata utepe na kutawazwa bingwa mwaka huu wa mbio za London Marathon.

Tigist Tufa wa Ethiopia, aliyeshinda mwaka jana, safari hii amekuwa wa pili.

Mkenya mwengine Florence Kiplagat alimaliza katika nafasi ya tatu akitumia muda wa saa mbili dakika 23 na sekunde 39

NAPE AZINDUA TAMASHA LA KIMATAIFA LA FILAMU MJINI ARUSHA

 Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza wakati wa uzinduzi wa tamasha la Kimataifa la Filamu la Tanzanite mkoani Arusha .

 Waziri Nape aliwaambia wadau na waigizaji wa Filamu waliohudhuria uzinduzi wa Tamasha hilo kuwa hii ni moja ya hatua kubwa kwenye historia ya filamu nchini na kuahidi Wizara yake itaendelea kutoa ushirikiano mkubwa na kuhakikisha haki za wasanii hazipotei wala haziliwi na wajanja.

 

 Mkurugenzi wa Tanzanite One ambao ndio wadhamini wakuu wa Tamasha, Ndugu Faisal Juma akizungumza wakati wa uzinduzi wa Tamasha la Kimataifa la Filamu la Tanzanite mjini Arusha kwenye hotel ya Mt. Meru

  Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akifunua pazia kuashiria uzinduzi wa Tamasha la kimataifa la filamu la Tanzanite mjini Arusha.

  Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye (mwenye kaunda suti ya kijivu) akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ndugu Felix Ntibenda  kwenye picha ya pamoja na viongozi pamoja na wadhamini kwenye uzinduzi wa Tamasha la Kimataifa la Filamu la Tanzanite.

 Viongozi wa Arusha wakiwa

 Baadhi ya watu waliohudhuria uzinduzi huo wa Tamasha la Filamu la Kimataifa la Tanzanite.

Yvonne Cherry 'Monalisa' pamoja na mama yake, Suzan Lewis 'Natasha' (katikati) wakifuatilia sherehe uzinduzi wa Tamasha la Filamu la Kimataifa la Tanzanite kwenye hotel ya Mt. 

UKIMYA WA UPINZANI BUNGENI MASHAKA KWA WASOMI



UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu wakati wa mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, umechukuliwa kwa hadhari kuwa unaweza kusababisha kambi hiyo ionekane inalinda posho bungeni.

Hadhari hiyo imetolewa na wasomi na viongozi mbalimbali waliozungumza na gazeti hili jana, walipokuwa wakitoa maoni kuhusu uamuzi wa kambi hiyo kususa hotuba hiyo.

Dk Bana

Mhadhiri wa fani ya siasa na utawala katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk Benson Bana, ndiye aliyesema kuwa kama uamuzi huo wa kuwa bubu bungeni hautabadilishwa, kambi hiyo itaonekana inalinda posho na kwamba haipo kwa ajili ya kutetea wananchi.

“Kazi yao ni kuwakilisha wananchi na makundi yote bungeni, sasa kitendo cha kuota ububu na kushindwa kueleza kero za wananchi, ni kutotendea haki wananchi maana ni vema wakae bungeni na kutoa hoja zao la sivyo, itafika wakati watatuomba radhi wananchi,” alisisitiza.

Akizungumzia hoja ya kwanza ya Mwenyekiti wa kambi hiyo, Mbunge wa Hai, Freeman Mbowe (Chadema), kulalamikia muundo wa Serikali kutowekwa gazetini, Dk Bana alihoji kama Mbowe hajui kuwa muundo wa Serikali hautolewi kwa kila mtu.

Kuhusu suala la fedha zilizokatwa katika Mfuko wa Bunge na kuelekezwa katika utengenezaji wa madawati, Dk Bana aliwashangaa wawakilishi hao wa wananchi wanaopingana na uamuzi wa kumuinua mwananchi wa kawaida.

Alisema wananchi wote walipendezwa na hatua hiyo ya Serikali ya kuchukua fedha zilizotoka bungeni baada ya kubana matumizi na kupeleka katika kununua madawati.

“Hatua hii ni kielelezo kuwa Bunge lilikuwa likipangiwa fedha nyingi kuliko matumizi yake hivyo kusababisha kuwepo matumizi ya hovyo, sasa viongozi wa Bunge kuliona hilo na kurejeshwa kwenye jamii ni jambo jema,” alisema.

Alionya kuwa mikakati ya kambi ya upinzani, ni kutetea wananchi lakini kwenye hilo wananchi wenyewe kila kona wanawashangaa kwani inaonesha kutetea maslahi ya wabunge.

Bashiru Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Bashiru Ally alisema wananchi wanaangalia vitendo vya wabunge wao ndani ya Bunge na watawahukumu kwani michango yao ndani ya Bunge ni muhimu na njia ya kutatua tatizo si kususa, bali kufuata taratibu za kisheria.

Alisema uamuzi wa kutozungumza, unaondoa maana ya vyama vya upinzani ndani ya Bunge kwa kuwa watashindwa kujadili masuala yenye manufaa ya wananchi, kwani mawazo ya kiongozi wa upinzani bungeni ni muhimu na yanawekwa kwenye kumbukumbu.

“Kuwekwa kwenye kumbukumbu mawazo hayo ni kwa ajili ya vizazi vijavyo, sasa kitendo cha Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni kutumia vibaya nafasi anayopewa, ni udhaifu wa kimkakati,” alisisitiza Bashiru.

Shehe Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum, alisema wanavyofanya wapinzani ni jambo lisilopendeza katika kuleta umoja wa kitaifa, kwani wao ni wawakilishi wa wananchi ndani ya Bunge na kususa siyo jambo la kiungwana.

TWITTER YAMTIA NDANI MWANDISHI


Polisi nchini Uturuki wamekamata mwandishi wa habari aliyemkosoa rais wa nchi hiyo kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter.

Ebru Umar raia wa Uholanzi alikamatwa na polisi baada ya kumkosoa rais Recep Tayyip Erdogan alikamatwa katika mji wa wa magharibi wa Kusadasi jumamosi usiku.

Wizara ya maswala ya nje ya Uholanzi imethibitisha kuwa Bi Umar alichapisha ripoti iliyomkosoa Sera za rais Erdogan ya kuwataka watu wote wenye asili ya Uturuki kuripoti wakati wowote mtu anapomtusi au kumkosoa nchini Uholanzi.

Hapo jana rais wa baraza kuu la muungano wa ulaya Donald Tusk, aliitaka serikali iruhusu uhuru wa kujieleza kama inavyotakikana kikatiba itakelezwe.

Tusk ambaye alikuwa ameandamana na waziri mkuu Ahmet Davutoğlu alionya kuwa uhuru wa wanahabari unatishiwa na maamuzi ya wanasiasa wachache serikalini.

Bw Davutoğlu kwa upande wake ameamua kutetea rekodi ya Uturuki, kuhusiana na uhuru wa vyombo vya habari, katika kikao na waandishi habari kilichohudhuriwa na Bi Merkel na maafisa wakuu wa jumuia ya muungano wa bara Ulaya.

Rais wa baraza kuu la muungano wa jumuia ya EU Donald Tusk, alidokeza kuwa, wanasiasa wanafaa kuamua kuhusiana na swala la ukosoaji na uharibifu wa hadhi ya mtu, hasa kuhusiana na ukiukaji wa haki ya uhuru wa kujieleza kwa vyombo vya habari.

Baadhi ya wanahabari wa Uturuki wamefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kutoa siri za serikali.

Mwezi uliopita, gazeti kuu linaloandika maswala ya upinzani - Zaman, lilishuhudia wanachama wa halmashauri kuu ya usimamizi, wakifutwa kazi na mahala pao kujazwa na waandishi, wanaounga mkono serikali.

Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan pia, amekuwa akitathmini kuwasilisha mashtaka dhidi ya muigizaji wa kuchekesha, raia wa Ujerumani, ambaye alitoa matamshi ya kumkejeli.

BURIANI PAPA WEMBA

Nyota wa muziki wa Soukous ambaye ni raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo- Papa Wemba amefariki dunia

Papa Wemba ambaye jina lake halisi ni Jules Shungu Wembadio Pene Kikumba, alianguka na kufa jukwaani akiwatumbuiza maelfu kwa maelfu ya mashabiki wake waliojitokeza katika tamasha la muziki mjini Abidjan Ivory Coast.

Gwiji huyo wa muziki wa lingala alizaliwa mnamo Juni 14 mwaka 1949, katika eneo la Lubefu - Wilaya ya Sankuru nchini Congo.

Alikuwa maarufu katika micharazo ya muziki wa Soukous,

Alikuwa mmoja kati ya wanamuziki maarufu sana barani Afrika na kote duniani.

Msanii huyo nguli mwenye sauti ya kumtoa nyoka pangoni anasemekana alianza kutetemeka, kisha akaanguka na kuzirai, alipokuwa akitumbuiza jukwaani Abidjan.

Papa Wemba, kama alivyofahamika na mashabiki wake, alikuwa na umri wa miaka 66 na alikuwa amepata uraia wa Ubelgiji.

Vibao vyake ni kama Mwasi,show me the way, Yolele, Mama,Proclamation"Chouchouna" (Papa Wemba), "Eluzam" na " Mbeya Mbeya" (Evoloko Lay Lay), "BP ya Munu" (Efonge Gina), "Mwana Wabi" , "Mizou" (Bimi Ombale) , "Zania" (Mavuela Somo.