• This is Slide 1 Title

    This is slide 1 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 2 Title

    This is slide 2 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 3 Title

    This is slide 3 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

Friday, March 20, 2015

AFUMANIWA AKILA URODA NA NG'OMBE



Wanakijiji wafurika katika boma hilo eneo la mugomoine, kiambaa huko Kenya wakishuhudia tukio hilo la kustaajabisha, jamaa adaiwa kufumaniwa akifanya ngono na ng’ombe mashahidi wadai kumuona akiwa anapanga mawe ili kufikia urefu kasha kuvua nguo na kuanza kufanya kitendo hiko cha kikatili.
Baada ya mjadala kuzuka kwanini jamaa huyo mshtakiwa ambaye jina lake limehifadiwa kumchagu ng’ombe huyo ndipo mama mmoja miongoni mwa mashuhuda asema kuwa ng’ombe huyo alikuwa mja mzito labda ndicho kilicho mvutia mshtakiwa, na je jamaa alijuaje kuwa ng’ombe Yule ni mja mzito..?

Wananchi waliokuwa na hasira walitaka kumpa kichapo mithili ya mbwa mwitu lakini punde askari nao wakawa wamewasili eneo la tukio na kumchukua mtuhumiwa huyo kwa ajili ya hatua za kisheria kuchukuliwa, lakini mstakiwa hakukubali mashtaka hayo.

JE UMETOBOA SEHEMU ZA SIRI


Wanawake wote walioamua kupamba sehemu zao za siri kwa kuzitoboa wanachukuliwa kuwa wamepitia ukatili wa kijinsia ama wamekeketwa kitengo cha afya kimetanabahisha hayo. Hata kama mtu huyo amefikia umri wa utu uzima na ameyafanya hayo kwa ridhaa yake,bado atahesabika kuwa alipitia ukatili wenye madhara kwa afya yake,na inapaswa kuchukua tahadhari kubwa kuweka kumbu kumbu za watu walio toboa sehemu zao za siri.
Lakini kujichora mwilini maarufu kama Tattoo ama kutoboa sehemu za siri ama mwilini,kumepingwa na taasisi ya utoboaji na uchoraji tattoo mwilini kwamba hakuna uhusiano wowote na ukeketaji. Na kueleza kuwa vitu hivyo viwili havichangamani kulinganisha na kutoboa sehemu za mwili wa mwanadamu,na taasisi hiyo wanachukulia suala la kutoboa mwili kama jambo la kaiwada na la ridhaa anasema msemaji wa taasisi hiyo Marcus Henderson.
Zaidi ya matukio ya ukeketaji yapatayo mia mbili yalichunguzwa na polisi wa kimataifa miaka mitano iliyopita,na inashauriwa kama kuna mtu mmoja ana mashaka na suala ya ukeketaji wataarifu polisi. Watoboaji makini huwa hawataki kuumiza wateja wao na huwa hawataki kuonesha tundu za kazi zao na hawako tayari kumtoboa mtu aliye chini ya umri wa miaka kumi na nane,anaeleza Mr Henderson.
 
Mtoboaji maarufu amesema kwamba wateja wengi wanataka kutobolewa sehemu zao za siri 

Mtoboaji maarufu kutoka mjini London ambaye ametaka ahifadhiwe jina lake, amesema kwamba wateja walio wengi huwa wanataka kutobolewa sehemu zao za siri zisilingane na ukeketaji.
Sihusiki na ukeketaji,nadhani utoboaji ni zaidi ya pambo mwilini ama uvumbuzi mpya wa kihisia zaidi.
Mtoboaji huyu anadai kwamba huwa anaitekeleza kazi yake kwa ufanisi mkubwa,kwanza huangalia picha kwa umakini mkubwa kabla hajamtoboa mtu, na kamwe hawezi kumtoboa mtu aliye na umri wa chini ya miaka kumi na nane.
Na wateja wake walio wengi ni wanawake na hutoboa sehemu ya siri hasa kwenye pezi la sehemu ya kati ya maungo ya mwanamke.
Ingawa mtoboaji huyu mashuhuri mwanzoni alikuwa hakubali kutoboa sehemu za siri za wanawake,na hii ni kutokana na maungo hao yalivyo na hatari inayowakabili kupitia utaratibu huo.
Naye msemaji kutoka kitengo cha afya ambaye ni mwanamke anasema kwamba,kuna changamoto kwa baadhi ya maeneo wanawake watu wazima hutobolewa sehemu zao za siri kilazima na maeneo mengine wasichana hulazimishwa kutobolewa.
Wanawake waliotoboa sehemu zao za siri watachukuliwa kuwa wamepitia ukatili ama wamekeketwa
Idadi ya wanawake waliokeketwa nchini Uingereza inatajwa kufikia laki moja na elfu sabini,na zaidi ya wanawake na wasichana elfu mbili na mia sita wamehudumiwa na kitabibu tangu September na kati ya hao ,mia nne tisini na tisa walitambuliwa January mwaka huu pekee.
Nayo serikali ya Uingereza imesema kwamba haina mpango wa kuifanyia marekebisho sheria ya mwaka 2003 kuingiza suala la kufanya upasuaji kwa masuala ya urembo kwenye sehemu za siri.
Kamati teule ya wabunge katika taarifa yake imesema kwamba sheria hiyo haina budi kubadilishwa ili kuweka wazi juu ya taratibu hizo kuwa ni kinyume cha sheria na zaidi ni kosa la jinai kama zitafanywa kwa msichana wa chini ya miaka kumi na nane isipokuwa kwa sababu ya afya ya akili au kimwili.
abari kutoka BBC

Je uliandika lini mwisho barua ya Mahaba ?



 Idhaa ya utangazaji ya BBC leo imezindua mradi wa kitaifa unaohusisha wanafunzi katika utangazaji wa habari.
Wanafunzi kutoka maeneo mbalimbali ya dunia wamepata fursa ya kuandaa ripoti kuhusu maswala mbalilmbali yanayowahusu. Kutoka mji mkuu wa Kenya Nairobi tunakuletea ripoti iliyoandaliwa na wanafunzi wa shule ya upili ya wavulana ya Starehe ambapo hawaruhusiwi kubeba simu za mkononi shuleni.
Karibu katika shule ya Starehe boys centre mjini Nairobi. Shule yetu inajulikana kwa umahiri katika masomo hasa katika mitihani ya kitaifa.


Ili kuimarisha umakinifu wetu masomoni, haturuhisiwi kubeba simu shuleni.
Tuna vyumba vya computa vyenye internet lakini tunavitumia tu kwa masomo na utafiti peke yake.
Haturuhusiwi kutumia computa kwa mawasiliano kupitia barua pepe au mitandao ya kijamii kama vile Facebook na Twitter.
Lakini hilo halituzuii kuwasiliana na marafiki zetu hasa wasichana katika shule zingine.


Matumizi ya simu yamepelekea watu wengi kusahau uandishi wa barua
Inatubidi kutumia njia ya zamani,tunaandika barua,lakini sio barua za kawaida.
Ni barua zilizoandikwa kwa umakinifu na kurembeshwa kwa kalamu zenye rangi aina mbalimbali na hua tunaziandika wakati wa mapumziko.
Katika maktaba ya shule nakutana na baadhi ya marafiki zangu wakiandika barua baada ya masomo.
''Mara nyingi tunaandika barua hizi kwa marafiki zetu wasichana kwa hivyo tunaziandika kwa njia spesheli ili kupasha hisia zetu sawasawa'', anasema Charles huku akitabasamu.
Baadhi ya wanafunzi wanaamini kuandika barua ni njia bora kwani inawapa fursa kutumia vipaji vya usanii.''
Napenda sana sanaa ya uchoraji na pia matumizi ya lugha hasa ya mapenzi '', anasema Moses huku akirembesha bahasha kwa kutumia kalamu zenye rangi tofauti.
Kwa mpenzi wangu ....
''Namwandikia rafiki yangu wa karibu sana nilimuona mara ya mwisho wakati wa likizo na nahisi nimemkosa sana'', anaongeza.
Baada ya kuandika barua hizo, tarishi anatumia pikipiki yake kuzisafirisha hadi katika shule ya wasichana ya Loreto Msongari, upande mwingine wa mji.
Wasichana wanafurahia kuzipokea na baadhi yao wananieleza fikra zao kuhusu matumizi ya barua kama njia ya kuwasiliana.


''Nimependezwa sana na barua niliyopokea ,imerembeshwa kwa rangi aina mbalimbali'' anasema Stacy.
'' Nafikiri ni bora kutumia barua kuwasiliana kwasababu njia zingine kama simu zinaweza kutufanya tusizingatie masomo'', anaongeza.
Wasichana kutoka shule jirani wakisoma barua kutoka kwa wapenzi wao katika shule ya Starehe
Naye Stephanie aliniarifu kuwa alifurahishwa sana na barua aliyopokea, '' alinifurahisha sana naona alitumia lugha safi sana, naona tuendelee matumizi ya barua'', anasema.
Nilimtaka msichana Angel kunieleza kilichomvutia zaidi katika barua aliyopokea.
'' Nilifurahia pale aliponiambia kuwa nywele zangu ndefu zinapendeza na kwamba nina tabasamu ya kuvutia kiasi kwamba inaweza kumfanya awe kipofu'' anasema huku akicheka.
Huku vijana wengine duniani wakiwasiliana na marafiki zao kwa kutumia simu za mkononi imebidi sisi kutumia mbinu ya kuandika barua kufanya hivyo na inatufaa na kutufurahisha

Habari kutoka BBC

UJUMBE WA WhatsApp WASABABISHA TALAKA

Mwanamume mmoja nchini Saudia amempa talaka mkewe kutokana na ujumbe wake katika mtandao wa WhatsApp. Kulingana na gazeti moja la kiharibu Al Hayat, mwanamume huyo amedai kwamba mkewe aliandika ujumbe unaosema ''naomba kuwa na subra ya kutosha ili kuweza kuishi na wewe''.

''Nilimpigia mmoja ya ndugu zangu kumuuliza iwapo ujumbe ule ulikuwa unanilenga mimi'', alisema mwanamume huyo.Watu wa Familia yangu walithibitisha hilo na nilisikia aibu kubwa kwamba mabibi za marafiki zangu pamoja na watu wa familia yangu wanaona ninaaibishwa.Hata sielewi alikuwa akimaanisha nini''.Amesema kuwa ndo yake ilikuwa taabani na kwamba kitendo hicho hakikustahili kufanyika.Si mara ya kwanza amenichafulia jina katika mtandao wa kijamii.Niliamua kumpa talaka kabla ya kuyatamgaza maisha yangu katika mitandao ya kijamii.'',
Khalid Al Habibi ,naibu mkurugenzi wa kituo cha kijamii kinachojihusisha na watoto mayatima anasema kuwa mitandao ya kijamii ni chanzo kikuu cha talaka.

BWENI LA WATOTO WA KIKE LATEKETEA NA MOTO DAR



Tukio hilo lililotokea leo majira ya 2:35 asubuhi linadaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme  katika jingo hilo. Jengo  la ‘Block B’  la Hostel za Mabibo,  za wanafunzi wa kike wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam(UDSM), jijini hapa limeungua kwa moto na kuteketeza vifaa na mali kadhaa  za wanafunzi waliokuwa wakiishi kwenye jengo hilo. Tukio hilo lililotokea leo majira ya 2:35 asubuhi linadaiwa kusababishwa na hitilafu ya umeme  katika jingo hilo. Makamu Mkuu wa UDSM, Profesa Rwekaza Mukandala aliyekuwa eneo la tukio akiahidi kubeba dhamana ya kushughulikia hasara ya mali, nyaraka na fedha kwa wanafunzi walioathiriwa na tukio hilo.
“Kwanza kuhusu vyeti vilivyoungua ,tutashughulikia vipatikane vyote.Pili tutashughulikia hata bajeti za kujikimu kwa wale walioathirika, lakini pia kuanzia leo wanafunzi wote ambao walikuwa kwenye jengo hilo watahamishiwa jengo lingine wakati huo uchunguzi ukifanyika kufahamu chanzo cha moto,” alisema Profesa Mukandala. Kwa upande wake, Kamanda wa Mkoa wa Kinondoni, Camilius Wambura alitoa tahadhari ya usalama kwa mali za wanafunzi walioathiriwa na tukio hilo huku akisisiza utulivu wakati uchunguzi wa chanzo hicho ukifanyika. Taarifa kutoka miongoni mwa wanafunzi hao zimebainisha kuwa, wakati wa tukio hilo wanafunzi wawili wa kike waliruka kutoka gorofa ya pili mpaka chini na kujeruhiwa vibaya.
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) wakiangalia moja la bweni lililokuwa likiteketea leo katika hostel za Mabibo.  

Askari wa Zima Moto walifika eneo la tukio hilo saa 3:45 asubuhi na kukuta moto ukiwa umeshapungua hatua iliyosababisha wanafunzi hao kuwashambulia huku wakiwazomea  na kuwataka waondoke. Viongozi wawili wa zima Moto, Omary Katonga kutoka Ilala na Mboke Msami wamesema changamoto kubwa iliyojitokeza ni kutopata taarifa mapema.
“Moto umetokea saa 2:35 asubuhi kwa nini watujulishe tena kupitia Tanesco saa moja baadaye, tumefika hapa kwa kutumia dakika 23, wanakosea kutulaumu ila kinachotakiwa ni taarifa mapema,” amesema Katonga.