• This is Slide 1 Title

    This is slide 1 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 2 Title

    This is slide 2 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 3 Title

    This is slide 3 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

Sunday, August 31, 2014

JAY DEE KOMANDO ATOLEA UVIVU MAGAZETI YA UDAKU





Iko haja ya kuzingatia magazeti yanayo andika vitu visivyo na uchunguzi yakinifuu juu ya habari zinazotolewa. Hivi karibuni gazeti moja limeandika habari kumhusu Komando Lady Jay Dee ambazo hazikumfuraisha ndipo alipo amua kuonyesha ukomando wake kwa kufunguka juu ya ukweli wa habari ya kuwa ana toka na dogodogo. Kupitia mtandao wa kijamii Komando Jay Dee alifunguka yafuatayo…
“Zamani ilikuwa haipo sehemu ya kujitetea, gazeti likishaandika ndio limeandika. 
Lakini sasa ulimwengu umebadilika, sio muda wa watu wote kulishwa chakula kisichofaa. 
Kwanza hicho kichwa cha habari kimenivunjia heshma sana. Nafikiri lengo ni kuilazimisha jamii inayomuelewa JayDee tofauti imuone kuwa ni mtu asiefaa, sawa. Dogo anaswa na mkoko? Huo mkoko mmemnasa nao wapi wakati hizo picha ni mimi nilizi post mwezi February Instagram?
Picha ambazo zilipigwa Nyumbani lounge tena kutumia simu ya Gardner.
Jide, dogodogo gumzo mjini. Gumzo ni kitu kinachoongelewa sana na kilichoenea kila kona sasa hii habari ni gumzo wapi ambapo haisikiki.

Mngeandika tumeamua kumuanzishia Jide gumzo hili, ndio ningewaelewa. 
Vitu vya kuzua. Ni watu wengi tu wakija band wakipata nafasi wanaomba kupiga picha na mimi na wengine pia wanaomba kupiga picha na gari sababu wanaipenda. Kama mtu yoyote anavyoweza kupiga picha na sanamu la kitu chochote anachokipenda. Hivi je! Wimbo wa JayDee mgumba, JayDee tasa umechuja? Umeisha chati?? Nashangaa na najiuliza tu
Inawezekana wimbo huo umechuja ndio maana mnatafuta wimbo mwingine utakao hit zaidi ya ule. Ndio kinachopelekea kuandika story za namna hii. Sio nyinyi mliokuja kuomba radhi kwa yote mliowahi kuniandika na kudai kuwa mmejirekebisha, miezi kadhaa tu iliopita?
Sio boss wenu aliemfuata Gardner na kumwambia tumalize tofauti zetu? 
Kama hizo tofauti zilikuwepo Inawezekana nyie ndio mna tofauti na mimi, sijawahi kuwa na tofauti na mtu hata nisiemfahamu.

Nashukuru Mungu nilikataa msamaha wenu ni kama nilihisi hamkumaanisha au sababu sijawahi kukubali show mlizotaka kufanya na mimi? Je! Hiki ni kisasi? Sielewi Mungu alienisimamia ataendelea Hii sio vita ya kwanza wala ya mwisho Dunia ni mapambano.
Kama nia ni kufanya niishi maisha ya uoga, kudhoofika na msongo wa mawazo mmefeli wengine mkijidai ni wacha Mungu huku mkiumiza nafsi za watoto wa binadamu wenzenu. 
No wonder mnaishi bila amani mbali na utajiri mlionao kwa kuogopa visasi. Sikuzaliwa kukata tama pia wapo wanaopenda kuandikwa kwenye hayo magazeti yenu wafanyieni favor ya kuwapa hiyo nafasi mi sifanyi muziki wa magazeti ya udaku  mkiachana na mimi nitashukuru sana hata ndoa yangu ikivunjika haimaanishi mnitafutie story za kunichafua ndoa ya Madiba ilivunjika sembuse yangu nina utofauti ipi na binadamu wengine? Nyie ndoa zenu ziko perfect si ndio? 
Hewala watakatifu nyie, mnaoficha yenu na kutangaza ya wenzenu.

Mwisho nawaomba watu mnaonielewa kutoamini tu habari yoyote ambayo haijatoka kwangu wala kwa muwakilishi wangu ambae ni "Webiro Wakazi Wasira".
Kama kuna chochote cha watu kujua nitakiongea mimi kwa mdomo wangu sio kuwekewa maneno mdomoni. Kila siku ooooh tulimpigia simu hapatikani, namba yangu yenyewe kwanza hata mnaijua? Mngekuwa mnaijua msingekuwa mnahangaika mnawapigia watu wangu wa karibu kunitafuta , na hao watu hawawezi kunisaliti ndio sababu mpaka miaka 70 mtaishia kusema tulimpigia simu JayDee hapatikani. Nyie muongee chochote mnachojiskia Ila sie hatuna haki kujitetea? Hili nalo litapita kama mengine  Na inshallah nitakuwa hapa hapa nimesimama nawaangalia, Picha moja wapo ni hiyo ambapo mtoto wa vitoto alikuja siku hiyo hiyo na akapiga picha na Gardner, mbele ya gari hiyo hiyo mnayodanganya watu kuwa mmemkuta nayo na mahala ni hapo hapo Nyumbani Lounge, ,,,,, na picha nyingine ni hizo nilizowahi kuzi post mimi mwenyewe mwezi february leo zinanihukumu endeleeni kudanganya jamii Na hizo ni chat alizoniandikia huyo mtoto wa vitoto ambae ndio ilikuwa mara yangu ya kwanza kumuona na sijawahi kumuona tena. . Zaidi ya kuongea nae twitter ,,, sisemi kama mimi malaika lakini
Ukweli huwa hauchanganywi na uongo Kwa hili mmenidhalilisha sana 
Kama nia yenu jamii inione mwanamke nisiefaa na ninaependa dogodogo Basi Mungu atawaonyesha ukuu wake”..