• This is Slide 1 Title

    This is slide 1 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 2 Title

    This is slide 2 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 3 Title

    This is slide 3 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

Monday, May 2, 2016

GETRUDE CLEMENT AREJEA: BUNGE LAMKARIBISHA


Getrude Clement mwenye umri wa miaka 16 ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu anayesoma shule ya Sekondari Mnarani iliyopo jijini Mwanza, leo amepata nafasi ya kufika bungeni Dodoma baada ya kupewa mwaliko wa Serikali 

Hivi karibuni Getrude  alihutubia viongozi mbalimbali wa dunia kwenye mkutano wa Umoja wa Mataifa uliohusu mabadiliko ya tabia nchiuliofanyika New York Marekani ambapo leo Bungeni  amewahimiza Watanzania kutunza mazingira na kufuata maelekezo yanayotolewa na Serikali na wataalamu wa mazingira ili kuyatunza mazingira wanamoishi.

Getrude amesema kuwa amefarijika kwa kuwawakilisha vijana wa Tanzania na dunia kwenye mkutano wa mabadiliko ya tabia nchi ambapo mataifa 175 yalikutana kusaini makubaliano ya Paris.

Katika kuwahimiza vijana kujenga tabia ya kutunza mazingira, Getrude amewaasa vijana hasa wanafunzi kusimamia suala la utunzaji wa mazingira wakiwa shuleni kwa kwa kujiunga na klabu mbalimbali ambapo yeye amejiunga na klabu ya “Mali Hai” iliyopo shuleni anaposoma.

Kwa upande wa Watanzania kwa ujumla kwenye utunzaji wa mazingira, Getrude amesema kuwa ni vema wajifunze kutoka mataifa mengine yanavyosimamia utunzaji wa mazingira hasa matumizi ya mifuko ya plastiki.

Mwanafunzi huyo amekaribishwa na kutambulishwa kwa wabunge leo mjini Dodoma kwa heshima ya kuliwakilisha vema taifa wakati wa utiaji saini makubaliano ya namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki moon alimkaribisha Getrude kwa viongozi hao na kusema “Ni furaha yangu kumualika Getrude Clement ambaye pia ni mwakilishi wa vijana anayeishi Tanzania na anaziwakilisha sauti za vijana”.

MWALIMU AKIMBIA NA MSHAHARA WA MWAKA

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dk. Kebwe Stephen Kebwe ameamuru kukamatwa kwa Mwalimu Hamisi Salumu Mkoleme kwa tuhuma za kulipwa mishahara ya mwaka mmoja na nusu bila kufanya kazi katika kituo chake alichopangiwa baada ya uhamisho kutoka mkoa wa Tanga kwenda mkoa wa Morogoro bila kuripoti katika kituo alichopangiwa.

Akizungumza na walimu waliofika katika ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Mvomero ili kuhakikiwa Mkuu huyo wa Mkoa wa Morogoro Dokta Kebwe Stephen Kebwe ameitaka kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Mvomero kusimamia kwa ukamilifu zoezi hilo ikiwa ni pamoja na wafanyakazi wenyewe kutoa ushirikiano katika zoezi hilo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Betty Mkwasa amesema wameamua kuchukua hatua za kupitia upya orodha aliyokabidhiwa na Halmashauri ili kujiridhisha na kwamba iwapo itabainika mwalimu yeyote amefanya kosa kama hilo, hatua kali zitachukuliwa.

Mzazi wa watoto watatu aomba msaada; Pumu yamuandama



MKAZI wa Kijiji cha Mapinduzi Kata ya Kigwe Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma

Julietha Sokoine (24) ambaye amejifungua watoto wa watatu na ameiomba serikali,taasisi,mashirika  na watu binafsi kumpatia msaada wa kifedha utakaomsaidia kuwatunza watoto hao.

 Pia alisema msaada huo pia utamuwezesha kupata tiba ya ugonjwa wa pumu

ambao umemsababisha kuvimba mwili wote.

 Akizungumza mwishoni mwa wiki, Sokoine ameiomba jamii kumsaidia kutokana na

kukabiliwa na tatizo la ugonjwa wa pumu ambao pia umesababishia kuwa na

hali ngumu ya kimaisha ambayo inayomfanya kushindwa kuwatunza vizuri watoto

wake hao.

 Alisema watoto hao, Daniel Sokoine,David Sokoine na Davis Sokoine

walizaliwa kwa pamoja Machi 22, mwaka huu katika hospitali ya mkoa wa

Dodoma huku kati ya wawili wa wakiwa na uzito kilo mbili na nusu na wa

mwisho kilo mbili.

  “Hali yangu siyo mzuri kutokana na mimi mwenyewe kukabiliwa na tatizo la

ugonjwa wa pumu,ambao pia wakati mwingine ninalazimika kuwanywesha maziwa

ya ngombe watoto hao pindi ninapozidiwa na ugonjwa huo”alisema .

 Kwa upande wake baba wa watoto hao Sokoine Chipanta alisema pamoja na

juhudi nilizofanya za kilimo hata hivyo mazao yalinyauka na jua.

 Alisema kutokana na hali hiyo analazimika kutafuta vibarua ili kuweza

kupata fedha kwa ajili ya kununua chakula pamoja na matunzo ya watoto hao.

 Alisema kwa wale wote watakaoguswa na kuamua kumpa msaada wawasiliane naye

kwa namba ya simu 0652-744510.

Punyeto yamfukuzisha kazi Waziri wa Wizara ya Mawasiliano Enock Ruberangabo



Rais Jamhuri wa Kidemokrasi ya Congo, Joseph Kabila amemtimua kazi Naibu Waziri wa Posta na Mawasiliano kutokana na kusambaa kwa video inayomuonesha akipiga punyeto ofisini

Kwa mujibu wa televisheni ya taifa, RTNC, Kabila amedai waziri huyo, Enock Ruberangabo Sebineza ameliabisha taifa.
 

Tangu Alhamis iliyopita hadi Ijumaa, video hiyo imekuwa ikisambaa mtandaoni ikimuonesha waziri huyo akijichua ofisini kwake. Nyuma yake inaonekana bendera ya nchi hiyo na picha ya Rais Kabila.
 

Wananchi wengi wamekasirishwa na video hiyo na kumtaka ajiuzulu.