• This is Slide 1 Title

    This is slide 1 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 2 Title

    This is slide 2 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

  • This is Slide 3 Title

    This is slide 3 description. Go to Edit HTML and replace these sentences with your own words. This is a Blogger template by Lasantha - PremiumBloggerTemplates.com...

Friday, August 22, 2014

WAUAJI WA FORLEY MAREKANI YAWASAKA.



Ahadi ya Rais Barak Obama, Kuimarisha Ulinzi Marekani.
Kitengo cha sheria nchini Marekani kimeanza kufanya uchunguzi wa jinai dhidi ya kifo chamwandishi wa habari mwenye asili ya Marekani ,James Foley aliyeuawa na wapiganaji wa kiislamu wenye msimamo mkali. Mwanasheria mkuu wa kitengo hicho,Eric Holder ameweka wazi kuwa wote waliohusika na mauaji ya mwandishi huo watawatia mkononi muda si mrefu. Maofisa wa serikali ya Marekani wandai kwamba askari hao wauaji walidai kiasi kikubwa cha pesa zipatazo dola za kimarekani zaidi ya milioni mia moja na thelathini kama fidia ya kumuachilia James Foley.
Marekani imekwisha anza harakati za kuwasaka na hatimaye kuwakamata waliohusika na mauaji ya mwandishi huyo kwa kurusha ndege zake takriban sita katika anga inayomilikiwa na waislamu kaskazini mwa Iraq.pamoja na kwamba waislam hao kutishia kumuua mmarekani mwingine wanayemshikilia kama ulipizaji wa kisasi endapo mashambulio yataelemea upande wao.

AFISI ZA NFF ABUJA ZATEKETEA



Moto wateketeza afisi za NFF Abuja

Moto mkubwa umetekeza makao ya shirikisho la soka la Nigeria NFF iliyoko Abuja, moto uliowachukua zaidi ya saa mbili kuuzima huku wakisaidiana na umma kuuzima moto huo mkubwa . Afisa wa kuzima moto Eyo amesema kuwa wanashuku ya kwamba chanzo cha moto huo ulitokana na hitilafu ya umeme.
Katibu mkuu wa NFF bwana Musa Amadu amesema kuwa moto huo ulianzia katika afisi ya mhasibu wa shirikisho hilo.
"Niliwasili kama kawaida lakini nikakatazwa kupanda ghorofa kwani tayari moshi ulikuwa unafuka ''
"Wafanyikazi wa shirikisho hilo wangeweza kuzima moto huo lakini walishindwa kuingia ofisini humo na hivyo hawangfeweza kubaini chanzo kikamilifu''
''Hata hivyo nashukuru mungu kuwa hakuna mtu aliyepoteza maisha yake kutokana na moto huo kwahivyo hakuna faida ya kumlaumu mtu yeyote''
Mwenyekiti wa NFF Aminu Maigari anakumbwa na tuhuma za uongozi duni kutokana na mkasa huo wa moto ni pigo kwa shirikisho hilo ambalo tayari linakabiliwa na mvutano wa uongozi ambao umepelekea kung'olewa madarakani kwa mwenyekiti Aminu Maigari mara mbili akirejeshwa

KAMATI NDOGO YAUNDWA NA MWENYEKITI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA




Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samuel Sitta ameunda kamati ndogo yenye ujumbe wa watu 10 kwa ajili ya kushughulikia masuala ambayo  hayakufikia muafaka wakati wa majadiliano ya kupitia sura mbalimbali za Rasimu ya Katiba Mpya kwenye Kamati 12 za Bunge hilo.

Kamati hiyo itakuwa inaongozwa na Makamu Mwenyekiti wa Bunge hilo, Mhe. Samia Suluhu Hassan,ambapo  wajumbe  wa kamati hiyo wametoka kila pande ya Muungano  yaani watano wametoka Tanzania Bara na watano kutoka Zanzibar.

Aidha Mhe. Sitta akizungumzia kuhusu  maendeleo  ya kazi za Kamati  hizo, ambapo alisema zinaendele vizuri, hivyo kuanzia wiki ijayo sura zote 15 zitakuwa zimepigiwa kura,hivyo  Kamati hizo zitakuwa zimemaliza sura 17 ya rasimu hiyo na za nyongeza ifikapo Agosti 27,mwaka huu  ili kuanza kuwasilisha katika Bunge hilo kuanzia Septemba 2,mwaka huu.


Hayo yalisemwa leo na  Mhe. Samuel Sitta wakati akizungumza na waandishi wa habari alipokutana nao leo kuhusu muhtasari wa kikao cha Kamati ya Uongozi wa Bunge hilo kilichokaa leo kutathmini kazi za Kamati 12 za Bunge hilo lilipofikia pamoja kuridhia baadhi ya mapendekezo ya kuongeza Ibara na sura ndani Rasimu ya Katiba katika Kamati zao.
Mwenyekiti huyo aliyataja mambo ambayo yatashughulikiwa na kamati hiyo, ni muundo wa  Bunge  katika masuala  ya Muungano, uraia pacha, mahakama ya kadhi na kamati ya pamoja ya fedha.
“Haya mambo manne nimeagiza ufanyike utaratibu maalum,” alisema Mhe. Sitta.

 Mhe . Sitta  akizungumzia kuhusu tathimini ya mwenendo wa Kamati hizo, alisema zipendekeza masuala kadhaa na kuacha mengine  kama yalivyo katika rasimu hiyo.

Akizungumzia kuhusu yaliyojadiliwa katika kikao cha Kamati ya Uongozi ya Bunge hilo,kabla ya kukutana na waandishi wa habari, Mhe. Sitta alisema kamati hiyo imepokea mapendekezo kutoka katika kamati mbalimbali kuhusu kuongezeka kwa sura na Ibara za rasimu hiyo.

Aliyataja mapendekezo hayo , likiwemo la  Tume ya Marekebisho ya Katiba lililowasilisha na Jaji Warioba kuhusu ardhi, mazingira na rasilimali za taifa, Jumuia ya Tawala  za  Serikali za Mitaa (ALAT) na pendekezo la Haki ya Watumiaji huduma na bidhaa ili kuwalinda walaji lililowasilishwa , Hawa Ng’umbi  ambaye ni mjumbe wa Bunge hilo.

Aliyataja  mapendekezo  mengine  ni la  Jukumu la Serikali kujenga uchumi imara, ambapo lengo ni kuwa na maendeleo ya uchumi wa ujamaa na kujitegemea na Kuwepo kwa Baraza la Habari, la wajumbe wa 201 kuhusu ardhi, wafugaji, wavuvi pia na wachimbaji wadogo ili ziweze kutungwa Sheria za kusimamia masuala hayo.


Mhe. Sitta  alisema kutokana na mapendekezo  hayo kutakuwepo na ongezeko la ukurasa na sura kadhaa katika rasimu hiyo.

Alisema Kamati imebaini tatizo la mahudhurio,  aliwapongeza wajumbe wa Bunge hilo kutoka upande wa Zanzibar kwa kuwa na mahudhurio mazuri kwenye vikao kuliko kutoka  Tanzania Bara kuacha visingizio vya kutohudhuria vikao.

Katika hatua nyingine Mhe. Sitta alisema kutakuwepo na wataalamu  kabla ua kumalizika  kwa wiki hii kwa ajili ya kutoa ufafanuzi wa mambo  kadhaa kutoka Hazina kwa pande zote za Muungano, ambapo ataukuwepo pia Gavana wa Benki Kuu, Profesa Bonaventure Rutinwa kwa ajili ya suala la uraia pacha, uhamiaji  na Profesa Issa Shivji ambaye ataoa ufafanuzi juu ya aina ya Muungano ili kuwa na uwiano kwa kuwa hivi sasa yapo mambo machache. Imeandikwa na Magreth Kinabo, Dodoma  

MARIO BALOTELLI RASMI LIVERPOOL.





Klabu ya Liverpool imemsajili rasmi mshambuliaji machachari Mario Balotelli kwa jumla ya kiasi cha paundi milioni 16. Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers amesema kuwa wameamua kumchukua mshambuliaji huyo ili kuziba pengo lililoachwa wazi na Luis Suarez ambaye amehamia Barcelona. Balotelli ambaye mwaka jana alijiunga na timu ya AC millan kwa uhamisho wa paund milion 19 akitokea Machester City hadi sasa ameweza kufunga magoli 30 katika michezo 54. Balotelli alijiunga na Manchester City August 2010 kwa paundi milion 24 wakati huo akitokea Inter Milan ambako aliiwezesha klabu yake kuchukua kombe katika michuano ya ligiya England.

BOKO HARAM WATEKA CHUO CHA POLISI



Boko Haram wazidi kumlaza macho Raisi Jonathan Moyo


 
Kundi la wapiganaji la kiislam la Boko Haram,wamevamia shule moja ya mafunzo ya kipolisi kilichoko kwenye kitongoji cha Gwoza karibu na mpaka wa nchi ya Cameroon ambacho hufundisha maofisa wa Polisi nchini Nigeria.
Kikundi hicho cha Boko Haram pia kinasemekana kuudhibiti mji wa jirani na Gwoza uitwao Buni Yadi, shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch wametoa takwimu ya vifo vilivyosababishwa na kundi hilo kuua watu zaidi ya elfu kumi mpaka sasa tangu walipoanzisha harakati za kutaka upande wa kaskazini mwa Nigeria uwe chini ya utawala wa Kiislam.