Thursday, July 10, 2014

49 WAUWAWA BAADA YA NDEGE YA UKRANE KUTUNGULIWA




Wizara ya ulinzi inasema ndege hiyo ilikuwa ikikaribia kutua katika uwanja wa ndege wa Luhansk, Maafisa wa Ukraine wanasema  watu wanaopigana kujitenga na kujiunga na  Russia, wametungua ndege ya uchukuzi ya kijeshi na kuuwa watu wote 49 waliokuwa ndani ya ndege hiyo. Ofisi ya mwendesha mashataka mkuu huko Ukraine, ilisema wanajeshi 40 na wafanyakazi tisa waliuawa mapema leo Jumamosi  baada ya ndege hiyo ya jeshi la angani la Ukraine kupigwa risasi na kuanguka. Wizara ya ulinzi inasema ndege hiyo ilikuwa ikikaribia kutua katika uwanja wa ndege wa Luhansk ilipopigwa risasi. Ukanda wa video  unaonyesha mlipuko mkubwa karibu na uwanja huo wa ndege, unaoaminika kutoka kwa ndege  hiyo.

0 comments:

Post a Comment