Thursday, July 10, 2014

WATAFITI SOMALIA, UHARAMIA HUENDA UKAPUNGUA!



Utafiti wa hivi karibuni unaashiria kwamba uharamia kutoka pwani ya Somalia huenda ukapungua kwa kiwango kikubwa kwa kuwapatia wazee wa koo za kisomali njia mbadala za kujikimu kimaisha. Kwa mujibu wa ripoti ya utafiti huo wa chuo kikuu cha Oxford na King's College mjini London, iliyochapishwa katika jarida moja la Uingereza, Jamii huwalinda maharamia wakati hawana njia nyengne za kujipatia kipato.
Kwa sasa Jamii ya kimataifa inategemea mikakati iliyo ghali mno, zikiwemo meli za kijeshi kuzuia uhaharamia wa majini na kuweka njia za safari za majini kuwa salama .
Lakini utafiti huu unakubaliana na yale ambayo yamekuwa yakipendekezwa na wadau mbalimbali Afrika mashriki, kwamba suluhu la kudumu ni kujenga miundo mbinu kama vile bandari na barabara zitakazo wawezesha wanavijiji wa koo mbalimbali wanufaike kwa fursa za kibiashara halali, zitakazowawezesha kupata tiza za kuendeleza maisha yao.

0 comments:

Post a Comment