Sunday, May 10, 2015

POLISI HOI KWA KIPIGO, MBUNGE AKAMATWA

Loliondo. Polisi wawili, PC Isaack na PC Mabrouk wamejeruhiwa baada ya kupigwa na vijana wanaodaiwa kuwa ni Wamasai (morani) katika Kijiji cha Ololosokwani, Tarafa ya Loliondo wilayani Ngorongoro.
Tukio hilo pia limesababisha watu 25 kutiwa nguvuni, akiwamo mbunge wa zamani wa Jimbo la Ngorongoro, Merthew ole Timan na madiwani wawili.
Inadaiwa tukio hilo limetokana na kuchochewa na uhasama kati ya wananchi na polisi kutokana na migogoro ya ardhi katika wilaya hiyo, limesababisha PC Isaack kuvunjwa mkono na jana alihamishiwa Hospitali ya Seliani Arusha Medical Center kwa matibabu zaidi baada ya hali yake kuwa mbaya.
Mkuu wa Wilaya ya Ngorongoro, Hashimu Mgandilwa alisema watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya uchunguzi kukamilika.
“Ni kweli polisi wawili wamepigwa na jeshi liliendesha msako wa kuwatafuta watuhumiwa na kufanikiwa kuwakamata watu 25 kwa tuhuma za kushambulia polisi, uchochezi, kufanya mikusanyiko isiyo halali na kupanga mbinu za uhalifu,” alisema Mgandilwa.
Alisema chanzo cha kupigwa polisi ni operesheni ya kuchunguza wahamiaji haramu ambayo inapingwa na wananchi na viongozi wa eneo hilo.
Hata hivyo, viongozi waliokamatwa kuhusu tukio hilo, jana walipata dhamana.
Diwani wa Kata ya Ololosokwani, Iyanick Ndoinyo na Diwani wa Oldonyosambu Daniel Ngoitiko, walisema wanapinga tukio la kupigwa polisi hao, lakini chanzo ni polisi kukamata pikipiki za wananchi na kudai faini kubwa.
Iyanick alisema ingawa ni kweli kuna uhasama wa polisi na wananchi, lakini taarifa alizopata ni kwamba polisi wadai faini kubwa na kisha kumpiga kijana mmoja wa Kimasai.
“Sisi kama viongozi tunapinga kupigwa polisi, pia kukamatwa kwetu ni kudhalilishwa,” alisema.
Alisema, “Hatupingi hatua ya Serikali kuwaondoa wahamiaji haramu kutoka nchi jirani.”
Naye Ngoitiko alisema wao kama viongozi wanalaani tukio hilo na wanataka Serikali kufanya uchunguzi kujua chanzo badala ya kukamata watu bila kuwa na ushahidi.

Chanzo

Related Posts:

  • UDA: UCHUNGUZI UNAENDELEA Wakati Serikali ikiendelea kuchunguza mikataba kati ya Shirika la Usafiri Dar es Salaam (Uda) na Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka Dar es Salaam (Dart) kuhusu Mradi wa Mabasi Yaendayo Haraka (BRT), Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu… Read More
  • Deni la Taifa Lafikia Trilion 33. 5 Deni la Taifa limeongezeka kwa Sh7.05 trilioni, kutoka Sh26.49 trilioni Juni 30, 2014, hadi Sh33.54 trilioni sawa na ongezeko la asilimia 27. Kwa mujibu wa ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), … Read More
  • PICHA ZA UCHI ZAMFUNGA SIWEMA WA NEY WA MITEGO Wiki iliyopita zilianza kusikika taarifa mbalimbali kuhusu kuhukumiwa kwa mpenzi wa zamani na mama mtoto wa msanii Nay wa Mitego aliyehukumiwa kwenda jela miaka miwili  jijini  Mwanza. Pamoja na taari… Read More
  • UBAKAJI WA KITHIRI INCHINI Matukio ya ubakaji hasa kwa watoto wadogo yamekuwa yakiongezeka kwa kiwango kikubwa, ongezeko hili limebainika kutokana na ufuatiliaji tulioufanya kupitia matukio yaliyoripotiwa katika vituo vya Polisi ambapo katika kipi… Read More
  • Afisa Uchaguzi Halmashauri Ya Serengeti Ahukumiwa Miaka Saba Jela. AFISA uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara Bw.  Julius Bujabhi Makwasa amehukumiwa kifungo cha Miaka 7 jela baada ya kupatikana na hatia ya Makosa 34 yakiwepo ya Rushwa. Mnamo mwaka 2013 Taasi… Read More

0 comments:

Post a Comment