Saturday, April 23, 2016

MAKUBALIANO YA SYRIA MATATANI

Rais Barack Obama wa Marekani pamoja na mjumbe wa Umoja wa mataifa nchini Syria Staffan Di Mistura wamesema kuwa wanahofia kwamba makubaliano ya Syria huenda yakaanguka.

Katika ghasia za hivi karibuni,watu 18 wamefariki kufuatia mashambulio ya serikali mjini Aleppo huku ndege moja ya kivita ya Syria ikidaiwa kuanguka karibu na mji wa Damascus.

Akizungumza mjini Geneva ,Mistura amesema kuwa alitaka kuitisha mkutano wa kijimbo ili kunusuru makubaliano hayo.

Amesema kwamba watu 400,000 huenda wamefariki katika mzozo huo.

Mjumbe huyo wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa hana ushahidi wa idadi hiyo lakini akaongezea kuwa inakaribia

0 comments:

Post a Comment