Thursday, September 11, 2014

MAPANGO YA AMBONI TANGA NA Hi5 MAKALA



Tanga ni mkoa mmoja wapo unaopatikana hapa Tanzania ukiwa katika pwani ya Afrika mashariki ya Bahari ya Hindi. Ni kilometa mia tatu Hamsini ukitokea (350 KM) Dar-es-salaam hadi Tanga. Mkoa huu kwakeli una mambo mengi yakihistoria kati ya mikoa maarufu sana enzi hizo Tanzania huwezi kuacha kuutaja mkoa wa Tanga. Team Hi5 Media ilifanikiwa kutembelea mkoa wa Tanga ambapo ilitembelea maeneo mbalimbali ya kihistoria ikiwemo bandari kongwe ya Tanga, Mapango ya Amboni na kiwanda cha maziwa mpaka kule kwenye magofu ya kihistoria na katika kile kisiwa ambacho kinazama kinacho itwa Tongoni.


“YES GOOD BYE” ni maneno yaliyo tumiwa na bwana Osali Otango pindi alipokuwa akihudhuria mikutano ya wazungu pia alikazia kwa kusema “YOU WILL NEVER” pale wazungu wakikoloni walipo jadiliana jinsi ya kumkamata bwana huyu Osali Otango. Osali Otango alikuwa ni gwiji katika matumizi ya nguvu za giza mara zote alitafutwa na wakoloni wakizungu bila kupatikana. Osali Otango aliishi sehemu ya miujiza sehemu yakihistoria sehemu yenye mambo mengi ya kustaajabisha ambayo miaka milioni ishirini nyuma nazungumzia mapango ya amboni ama kwa jina la kisasa Amboni Caves. Mapango haya kwa sasa ni kivutio kikubwa cha utalii hapo mkoani Tanga. Katika mapango haya kuna mahali ambako watu walipatumia kuabudu na kufanya kafara wengi wao walikuwa ni makabila yanayo zunguka mapango haya yaani wazigua, wabondei pamoja na wadigo hapo zamani. Katika mapango haya kuna miamba inayo toka chini kwenda juu na inayotoka juu kuja chini kwa lugha ya kitaalamu wanajografia huita Slack tight na slug might pia kuna miamba inayo kutana na kutengeneza aina nyingine kabisa ambyo wanaiita Earth Pira.

Wanasema ukiyastaajabu ya musa utayaona ya firauni ndani ya mapango haya pana maumbo ya kijinsia, jinsia ya kike na jinsia ya kiume, pia kuna kiti cha asili kilicho chongwa na maji pamoja na kwato lakini pia ndani ya mapango haya kuna eneo ambalo dini ya kiislam na dini ya kikristo walikuwa wakipatumia kwa ajili ya kufanya ibada ama hakika mapango haya ni kivutio kikubwa sana.
Imeandikwa na Donald Mtani “The Super Voice” Hi5 Makala

0 comments:

Post a Comment