Tuesday, January 26, 2016

DENMARK KUPITISHA SHERIA MPYA YA WAHAMIAJI



Umoja wa mataifa umekosoa hatua iliyochukuliwa na bunge Danmark kupitisha sheria yenye utata ya inayojaribu kuwazuia wahamiaji kuingia katika taifa hilo.
Sheria hiyo inatoa ruhusa kwa mamlaka ya serikali kutaifisha baadhi ya mali za wahamiaji wapya ili kufidia gharama ya huduma watakazopata.Sheria hiyo pia inalazimisha wakimbizi kusubiri hadi miaka mitatu kabla ya kuleta familia zao nchini nchini Denmark.
Upigaji kura umekamilika, 81 wamepiga kura ya ndio na 27 wamepiga kura ya hapana kukataa muswada, kura moja imeharibika, mswada umekubaliwa na sasa utapelekwa kwa Waziri Mkuu.
Mbali na kuzuiwa kuingia nchini Denmarka sasa wakambizi watakaopenya na kuingia nchini humo sasa ni ruksa kwa serikali kutaifisha mali zao kwa lengo la kufidia gharama za kuwahudumia.
Aidha wakimbizi waliobahatika kuingia hawataruhusiwa kuleta familia hadi miaka mitatu itimie.

0 comments:

Post a Comment