Sunday, April 24, 2016

UGANDA: BOMBA LA MAFUTA KUPITIA TANZANIA


Uganda imeamua kujenga bomba la mafuta yake kupitia Tanzania na wala sio Kenya.

Awali taifa hilo la Afrika mashariki ambayo haijapakana na bahari ilikuwa imezungumzia nia ya kujenga bomba la mafuta yake kupitia Kenya lakini baada ya mkutano na rais wa Tanzania Joseph Pombe Magufuli, rais wa Uganda Yoweri Museveni wameibwaga Kenya.

Kenya ambayo imegundua mafuta Kaskazini mwa taifa hilo sasa haina budi kujiunga na uganda kupitishia mafuta yake Tanzania au ijenge bomba lake kupitia bandari ya Lamu.

Uganda imeelezea wasiwasi wa mabomba ya mafuta kushambuliwa na wanamgambo wa Alshabab kwani bomba hilo la kupitia Kenya linatazamiwa kutumia bandari ya Lamu.

Uganda ilitangaza uamuzi wake katika kongamano la viongozi wa muungano wa Afrika Mashariki uliokuwa mji mkuu wa Kampala.

Muungano huo unajumuisha Kenya, Tanzania, Burundi, Rwanda na Sudan Kusini.

Bomba hilo la mafuta litakwenda kilomita 1,400km kuanzia Hoima, hadi kwenye bandari ya Tanga.

Mradi huo utagharimu takriban dola bilioni $4 za Marekani.

Aidha ujenzi huo unatarajiwa kutoa nafasi za kazi 15,000 kwa vijana ambao wanatatizika sana na uhaba wa ajira.

Bomba hilo la mafuta litakwenda kilomita 1,400km kuanzia Hoima, hadi kwenye bandari ya Tanga.

Uganda inakisiwa kuwa na mapipa bilioni 6.5 bn ya mafuta yanayotarajiwa kuanza kuchimbwa mwaka wa 2018.

Kampuni ya mfuta ya Ufaransa Total, ile ya China CNOOC na ile ya Uingereza Tullow ndizo zinazomiliki leseni ya kuchimba na kusafisha mafuta nchini Uganda.

Kenya sasa imeamua kujenga bomba lake kufuatia uamuzi huo wa Uganda.

Related Posts:

  • Serikali ya China kudhibiti dini Chama cha kikoministi cha China kimepewa mamlaka ya kudhibiti dini nchini humo. Kiongozi wa Uchina, Xi Jinping, amesema makundi ya kidini lazima yakubali kudhibitiwa na chama cha kikoministi. Akizungumza katika mkutano wa s… Read More
  • Serikali ya China kudhibiti dini Chama cha kikoministi cha China kimepewa mamlaka ya kudhibiti dini nchini humo. Kiongozi wa Uchina, Xi Jinping, amesema makundi ya kidini lazima yakubali kudhibitiwa na chama cha kikoministi. Akizungumza katika mkutano wa s… Read More
  • Wakenya kinara katika London Marathon Mwanariadha mkenya Eliud Kipchoge nusura avunje rekodi ya duniaya mbio za Marathon alipoandikisha muda wa kasi zaidi katika mbio za London Marathon. Kipchoge wa Kenya,alihifadhi taji aliloshindwa mwaka uliopita alipoandikish… Read More
  • NAPE AZINDUA TAMASHA LA KIMATAIFA LA FILAMU MJINI ARUSHA  Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Nape Nnauye akizungumza wakati wa uzinduzi wa tamasha la Kimataifa la Filamu la Tanzanite mkoani Arusha .  Waziri Nape aliwaambia wadau na waigizaji wa Filamu wali… Read More
  • UKIMYA WA UPINZANI BUNGENI MASHAKA KWA WASOMI UAMUZI wa Kambi ya Upinzani bungeni kuingia katika vikao vya Bunge na kugeuka bubu wakati wa mjadala wa Hotuba ya Ofisi ya Waziri Mkuu, umechukuliwa kwa hadhari kuwa unaweza kusababisha kambi hiyo ionekane inalinda posho bu… Read More

0 comments:

Post a Comment